Check out the new design

ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی سوره: آل عمران   آیه:
إِذۡ هَمَّت طَّآئِفَتَانِ مِنكُمۡ أَن تَفۡشَلَا وَٱللَّهُ وَلِيُّهُمَاۗ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Kumbuka, ewe Mtume, yale mambo yaliyowahusu kina Banū Salimah na Banū Ḥārithah wakati walipowaza kurudi nyuma, wao na kiongozi wao, mnafiki Abdullāh bin Ubayy bin Salūl, kwa kuogopa kukutana na adui. Lakini Mwenyezi Mungu Aliwalinda na Akawahifadhi wakaenda pamoja na wewe wakimtegemea Mwenyezi Mungu. Na kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na wajitegemeze Waumini.
تفسیرهای عربی:
وَلَقَدۡ نَصَرَكُمُ ٱللَّهُ بِبَدۡرٖ وَأَنتُمۡ أَذِلَّةٞۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Hakika Mwenyezi Mungu Aliwanusuru nyinyi, enyi Waumini, katika Badr juu ya maadui zenu washirikina pamoja na uchache wa idadi yenu na vifaa vyenu. Kwa hivyo, muogopeni Mwenyezi Mungu kwa kutekeleza amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake, ili mpate kumshukuria neema Zake.
تفسیرهای عربی:
إِذۡ تَقُولُ لِلۡمُؤۡمِنِينَ أَلَن يَكۡفِيَكُمۡ أَن يُمِدَّكُمۡ رَبُّكُم بِثَلَٰثَةِ ءَالَٰفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ مُنزَلِينَ
Kumbuka, ewe Nabii, yale yaliyowahusu Masahaba wako kwenye vita vya Badr pindi walipoona uzito katika nafsi zao kwa kuwa Makureshi wamepata msaada wa kivita, na Sisi tukakuletea Wahyi uwaambie, «Kwani hauwatoshi msaada wa Mola wenu wa kuwaletea Malaika elfu tatu walioteremshwa kutoka mbinguni mpaka kwenye sehemu ya vita wakawa wanawapa moyo na wanapigana pamoja na nyinyi?»
تفسیرهای عربی:
بَلَىٰٓۚ إِن تَصۡبِرُواْ وَتَتَّقُواْ وَيَأۡتُوكُم مِّن فَوۡرِهِمۡ هَٰذَا يُمۡدِدۡكُمۡ رَبُّكُم بِخَمۡسَةِ ءَالَٰفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ مُسَوِّمِينَ
Ndio, unawatosha nyinyi msaada huu. Na kuna bishara nyingine kwenu, iwapo mtakuwa na subira ya kupambana na maadui zenu na mkamuogopa Mwenyezi Mungu kwa kuyatenda Aliyowamrisha na kuyaepuka Aliyowakataza. Na watakuja makafiri wa Maka kwa haraka kupigana na nyinyi, wakidhani kwamba wao watawamaliza. Mwenyezi Mungu Atawapa nyinyi msaada wa Malaika elfu tano wakiwa wamejitia alama zilizo wazi, wao na farasi wao.
تفسیرهای عربی:
وَمَا جَعَلَهُ ٱللَّهُ إِلَّا بُشۡرَىٰ لَكُمۡ وَلِتَطۡمَئِنَّ قُلُوبُكُم بِهِۦۗ وَمَا ٱلنَّصۡرُ إِلَّا مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ
Na Mwenyezi Mungu Hakuuleta msaada huu wa Malaika isipokuwa ni kwa ajili ya kuwapa bishara kwa msaada huo na ili nyoyo zenu zitulie na ziwe nzuri kwa ahadi ya Mwenyezi Mungu kwenu. Na msaada wa hakika unatoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye kushinda Ambaye Hashindwi, Mwenye hekima katika uendeshaji mambo Wake na matendo Yake.
تفسیرهای عربی:
لِيَقۡطَعَ طَرَفٗا مِّنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَوۡ يَكۡبِتَهُمۡ فَيَنقَلِبُواْ خَآئِبِينَ
Na ilikuwa nusura ya Mwenyezi Mungu katika vita vya Badr ni kwa ajili Apate kukiangamiza kikundi cha makafiri kwa kuuawa na yule atakayeokoka na kifo kati yao, basi atarudi akiwa na huzuni, upetwe na dhiki za nafsi yake na unaonekana kwake utwevu na aibu.
تفسیرهای عربی:
لَيۡسَ لَكَ مِنَ ٱلۡأَمۡرِ شَيۡءٌ أَوۡ يَتُوبَ عَلَيۡهِمۡ أَوۡ يُعَذِّبَهُمۡ فَإِنَّهُمۡ ظَٰلِمُونَ
Huna, ewe Mtume, katika mambo ya waja chochote kile. Bali mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Peke Yake, Asiyekuwa na mshirika. Na huenda, baadhi ya hawa waliokupiga vita, vifua vyao vikaufungukia Uislamu, wakasilimu na Mwenyezi Mungu Akazikubali toba zao. Na yule atakayesalia katika ukafiri wake, Mwenyezi Mungu Atamuadhibu duniani na Akhera kwa sababu ya udhalimu wake na uadui wake.
تفسیرهای عربی:
وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ يَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Ni vya Mwenyezi Mungu Pekee vilioko mbinguni na vilioko ardhini; Anamsamehe Amtakaye kati ya waja Wake kwa rehema Zake na Anamuadhibu Amtakaye kwa uadilifu Wake. Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasamehe madhambi ya waja Wake na ni Mwenye huruma kwao.
تفسیرهای عربی:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَأۡكُلُواْ ٱلرِّبَوٰٓاْ أَضۡعَٰفٗا مُّضَٰعَفَةٗۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo, tahadharini na aina zote za riba na msichukue katika mkopo zaidi ya rasilmali zenu, hata kama ni kidogo. Basi itakuwaje iwapo ziada hiyo itaongezeka kila ufikapo muda wa kulipa deni? Na muogopeni Mwenyezi Mungu kwa kujilazimisha kufuata Sheria Zake ili mpate kufaulu duniani na Akhera.
تفسیرهای عربی:
وَٱتَّقُواْ ٱلنَّارَ ٱلَّتِيٓ أُعِدَّتۡ لِلۡكَٰفِرِينَ
Na jiwekeeni kizuizi baina yenu na moto ambao umeandaliwa makafiri.
تفسیرهای عربی:
وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na mtiini Mwenyezi Mungu, enyi waumini, katika yale Aliyowaamrisha kwayo ya twaa nay ale Aliyowakataza nayo ya kula riba na mengineyo. Na mtiini Mtume ili mpate kurehemewa na msiiadhibiwe.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: آل عمران
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

مترجم: دکتر عبد الله محمد ابو بکر و شیخ ناصر خميس.

بستن