ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی آیه: (199) سوره: سوره آل عمران
وَإِنَّ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَمَن يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِمۡ خَٰشِعِينَ لِلَّهِ لَا يَشۡتَرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ
Baadhi ya waliopewa vitabu wanamuamini Mwenyezi Mungu kuwa ni Mola Mmoja na Mungu Mwenye kuabudiwa, wanaiamini Qur’ani mliyoteremshiwa nyinyi na Taurati na Injili walizoteremshiwa wao, hali ya kumdhalilikia Mwenyezi Mungu na kumnyenyekea. Hawazibadilishi aya za Mwenyezi Mungu kwa thamani ndogo ya takataka za duniani wala hawayafichi Aliyoyataremsha Mwenyezi Mungu na wala hawayapotoshi kama wanavyofanya wengineo miongoni mwa waliopewa Vitabu. Hao watapata thawabu kubwa mbele ya Mola wao Siku ya kukutana Naye, na watapewa malipo yao kamili, bila ya kupunguzwa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhesabu. Hakumshindi Yeye kuyadhibiti matendo yao na kuwahesabu wao kwayo.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (199) سوره: سوره آل عمران
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن