ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی آیه: (26) سوره: سوره ص
يَٰدَاوُۥدُ إِنَّا جَعَلۡنَٰكَ خَلِيفَةٗ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱحۡكُم بَيۡنَ ٱلنَّاسِ بِٱلۡحَقِّ وَلَا تَتَّبِعِ ٱلۡهَوَىٰ فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ يَضِلُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ لَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدُۢ بِمَا نَسُواْ يَوۡمَ ٱلۡحِسَابِ
Ewe Dāwūd! Sisi tumekufanya ni msimamizi ardhini na tumekupa mamlaka huko, basi hukumu baina ya watu kwa uadilifu na uchungaji haki, na usifuate matamanio katika kuhukumu, kwani hilo litakupotosha na Dini ya Mwenyezi Mungu na Sheria Yake, hakika wale wanaopotea njia ya Mwenyezi Mungu watapata adhabu ya uchungu humo Motoni, kwa kughafilika kwao na Siku ya kulipwa na kuhesabiwa. Katika haya pana ushauri kwa viongozi wahukumu kwa haki iliyoteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, wala wasipotoke nayo wakapotea njia Yake.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (26) سوره: سوره ص
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن