ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی آیه: (100) سوره: سوره مائده
قُل لَّا يَسۡتَوِي ٱلۡخَبِيثُ وَٱلطَّيِّبُ وَلَوۡ أَعۡجَبَكَ كَثۡرَةُ ٱلۡخَبِيثِۚ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ يَٰٓأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Sema, ewe Mtume, «Hakilingani kiovu na chema cha kila kitu»: Kafiri halingani na Muumini, mwenye kuasi halingani na mtiifu, mjinga halingani na mjuzi, na mwenye kufanya uzushi halingani na mwenye kufuata njia, na mali ya haramu hayalingani na ya halali, ingawa unakuvutia wewe, ewe binadamu, wingi wa viovu na idadi kubwa ya watu wake. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, enyi wenye akili bora, kwa kujiepusha na machafu na kufanya mazuri, mpate kufuzu kwa kulifikia lengo kubwa, nalo ni radhi ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kufaulu kupata Pepo.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (100) سوره: سوره مائده
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن