ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی آیه: (4) سوره: سوره مجادله
فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ شَهۡرَيۡنِ مُتَتَابِعَيۡنِ مِن قَبۡلِ أَن يَتَمَآسَّاۖ فَمَن لَّمۡ يَسۡتَطِعۡ فَإِطۡعَامُ سِتِّينَ مِسۡكِينٗاۚ ذَٰلِكَ لِتُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦۚ وَتِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِۗ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Na Asiyepata shingo ya kuiacha huru, basi lililo wajibu kwake ni kufunga miezi miwili iliyofuatana kabla hajamuundama mkewe. Na asiyeweza kufunga miezi miwili kwa udhuru wa kisheria, basi na awalishe masikini sitini chakula kinachowashibisha. Hayo tuliyoyaelezea nyinyi ya hukumu ya kujiharamishia mke wake kwa kumfananisha na mgongo wa mamake ni kwa sababu mmuamini Mwenyezi Mungu na mumfuate Mtume Wake na mfanye matendo yanayoambatana na Sheria ya Mwenyezi Mungu na muache yale ambayo mlikuwa mkiyafanya wakati mlipokuwa kwenye ujinga. Hukumu hizo zilizotajwa ndizo amri za Mwenyezi Mungu na mipaka Yake, basi msiikiuke. Na wenye kuzikataa watapata adhabu yenye uchungu.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (4) سوره: سوره مجادله
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن