ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی آیه: (25) سوره: سوره انعام
وَمِنۡهُم مَّن يَسۡتَمِعُ إِلَيۡكَۖ وَجَعَلۡنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ أَكِنَّةً أَن يَفۡقَهُوهُ وَفِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَقۡرٗاۚ وَإِن يَرَوۡاْ كُلَّ ءَايَةٖ لَّا يُؤۡمِنُواْ بِهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءُوكَ يُجَٰدِلُونَكَ يَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kati ya washirikina hawa kuna wanaokusikiliza usomapo Qur’ani, ewe Mtume, na isifike kwenye nyoyo zao. Kwa kuwa wao, kwa sababu ya kufuata matamanio yao, tumeweka vifuniko juu ya nyoyo zao wasipate kuifahamu Qur’ani. Na tumejaalia kwenye masikio yao uzito na uziwi, hayasikii wala hayafahamu chochote. Na wanapoziona dalili nyingi zenye kuonyesha ukweli wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hawaziamini. Na hata wakikujia , ewe Mtume, baada ya kuzishuhudia dalili zenye kuonesha ukweli wako, huwa wakisema wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu, «Haya tunayoyasikia si chochote isipokuwa ni ngano zinazohadithiwa na watu wa kale zisizo na ukweli.»
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (25) سوره: سوره انعام
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی. ترجمهٔ دکتر عبدالله محمد ابوبکر و شیخ ناصر خمیس.

بستن