Check out the new design

ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس * - لیست ترجمه ها


ترجمهٔ معانی سوره: فجر   آیه:

Al-Fajr

وَٱلۡفَجۡرِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa alfajiri
تفسیرهای عربی:
وَلَيَالٍ عَشۡرٖ
na masiku kumi ya kwanza ya Mfungotatu na kwa kile kilichoyafanya yawe matukufu,
تفسیرهای عربی:
وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ
kwa kila idadi igawanyikayo na isiyogawanyika,
تفسیرهای عربی:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ
kwa usiku upitapo na giza lake.
تفسیرهای عربی:
هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ
Kwani hakuna katika kiapo kiliyotajwa chenye kukinaisha kwa mwenye akili?
تفسیرهای عربی:
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Huoni, ewe Mtume, vipi Mola wako
تفسیرهای عربی:
إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ
Alivyoiangamiza kaumu ya Ād'. kabila la Irama lenye nguvu na majengo yaliyoinuliwa juu ya vipia,
تفسیرهای عربی:
ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ
ambalo hakukuumbwa mfano wake katika miji, kwa ukubwa wa miili na wingi wa nguvu?
تفسیرهای عربی:
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ
Na vipi Alivyowafanya Thamūd, kaumu ya Ṣāliḥ, ambao waliweza kuchonga jabali na kufanya nyumba ndani yake?
تفسیرهای عربی:
وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ
Na vipi Alivyomfanya Firauni, mfalme wa Misri, aliyekuwa na askari waliouhami ufalme wake na kuutilia nguvu.
تفسیرهای عربی:
ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Hawa ndio waliokitumia nguvu na kudhulumu mijini.
تفسیرهای عربی:
فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ
Wakaeneza humo, kwa dhuluma zao, uharibifu.
تفسیرهای عربی:
فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ
Mwenyezi Mungu Akawamiminia adhabu kali.
تفسیرهای عربی:
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ
Hakika Mola wako,ewe Mtume, Anamwangalia mwenye kumuasi kwa kumpa muhula kidogo, kisha Humpatiliza kwa uwezo na ushindi..
تفسیرهای عربی:
فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ
Huyu binadamu, Mola wake Anapompa mtihani wa neema, Anapomkunjulia riziki yake na kumpa maisha mazuri, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye ana cheo kwa Mola wake na huwa akisema :»Mola wangu Amenitukuza.»
تفسیرهای عربی:
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ
Na Anapomuonja na Akambania riziki yake, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye amefanywa mnyonge na Mwenyezi Mungu na huwa akisema: «Mola wangu Amenifanya mnyonge.».
تفسیرهای عربی:
كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ
Hali ya mambo si kama anavyodhania binadamu huyu, kwani mtu hutukuzwa kwa kumtii Mwenyzi Mungu na hufanywa mnyonge kwa kumuasi Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamwakirimu mayatima na kuwatendea wema.
تفسیرهای عربی:
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hamhimizani kulisha maskini.
تفسیرهای عربی:
وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا
Na mnakula haki za watu, katika kurithi, kwa pupa.
تفسیرهای عربی:
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا
Na mnapenda mali kupita kiasi.
تفسیرهای عربی:
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Basi hali zenu zisiwe namna hiyo. Kumbukeni pindi ardhi itakapotikiswa na kuvunjwavunjwa.
تفسیرهای عربی:
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na Akaja Mola wako kutoa uamuzi kwa waja Wake hali Malaika wamepiga safu.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: فجر
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمه‌ى سواحلى - عبد الله محمد و ناصر خميس - لیست ترجمه ها

مترجم: دکتر عبد الله محمد ابو بکر و شیخ ناصر خميس.

بستن