ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی آیه: (87) سوره: سوره يوسف
يَٰبَنِيَّ ٱذۡهَبُواْ فَتَحَسَّسُواْ مِن يُوسُفَ وَأَخِيهِ وَلَا تَاْيۡـَٔسُواْ مِن رَّوۡحِ ٱللَّهِۖ إِنَّهُۥ لَا يَاْيۡـَٔسُ مِن رَّوۡحِ ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡقَوۡمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye, wala msikate tamaa na faraji ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraji ya Mwenyezi Mungu isipo kuwa watu makafiri.
Na kuwa na imani na Mwenyezi Mungu ndio huhuisha matumaini. Kwa hivyo zile dhiki za moyo hazikuondoka kwa matarajio ya Yaa'qub kumrudia wanawe, na yakamtia katika moyo wake kuwa wangali wahai, na kwamba wakati wa kukutana nao ndio umefika. Akawaamrisha wanawe wende wakawatafute, akawaambia: Enyi wanangu! Rejeeni Misri muwe na kaka yenu, na mumtafute Yusuf na nduguye, muulize khabari zao kwa upole bila ya watu kujua. Wala msikate tamaa kwa Mwenyezi Mungu kuturehemu kwa kuwarudisha. Kwani hawakati tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu isipo kuwa wale wanao kanya.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (87) سوره: سوره يوسف
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن