ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی آیه: (207) سوره: سوره بقره
وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَشۡرِي نَفۡسَهُ ٱبۡتِغَآءَ مَرۡضَاتِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ رَءُوفُۢ بِٱلۡعِبَادِ
Na katika watu yupo ambaye huiuza nafsi yake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake.
Ni farka kubwa baina ya wanaafiki hawa na Waumini wa kweli ambao watayari kuuza nafsi zao kwa sababu ya kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu na kulitukuza Neno la Haki. Hawa ni kinyume na wale wa kwanza. Hawa wakitawalishwa madaraka kuendesha mambo ya watu inakuwa ni katika upole wa Mwenyezi Mungu kuwafanyia waja wake. Mwenyezi Mungu Mtukufu huwarehemu hao waja wema kwa kuwatawalisha watu wema ili awalinde na wenye shari.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (207) سوره: سوره بقره
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن