ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی آیه: (96) سوره: سوره آل عمران
إِنَّ أَوَّلَ بَيۡتٖ وُضِعَ لِلنَّاسِ لَلَّذِي بِبَكَّةَ مُبَارَكٗا وَهُدٗى لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hakika Nyumba ya kwanza walio wekewa watu kwa ibada ni ile iliyoko Bakka, (Makka) iliyo barikiwa na yenye uwongofu kwa walimwengu wote.
Katika kufuata mila ya Ibrahim ni kuelekea wakati wa Swala Nyumba aliyo ijenga, na kwenda kuhiji huko. Mwenyezi Mungu amebainisha hayo kwa kusema: Hakika Nyumba ya awali kwa ukongwe na utukufu aliyo ijaalia Mwenyezi Mungu iwe ni ya ibada kwa watu ni hiyo iliyoko Makka (au Bakka kama pia inavyoitwa). Nayo ina kheri nyingi na manufaa, na Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taa'la ameijaalia iwe na baraka. Nayo Nyumba hiyo ni pahali pa uwongofu kwa watu kwa kuhiji na kuelekea wakati wa Swala.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی آیه: (96) سوره: سوره آل عمران
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن