Check out the new design

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Eggo (nantino) ngo e Swahiliire - Abdullah Muhammad e Naasir Khamis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Simoore: Simoore Yuusuf   Aaya:
وَٱتَّبَعۡتُ مِلَّةَ ءَابَآءِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ مَا كَانَ لَنَآ أَن نُّشۡرِكَ بِٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۚ ذَٰلِكَ مِن فَضۡلِ ٱللَّهِ عَلَيۡنَا وَعَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَشۡكُرُونَ
«Na nimefuata Dini ya baba zangu: Ibrāhīm, Is’ḥāq na Ya’qūb, ndipo nikaamuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake. Haikuwa kwetu sisi kumfanyia Mwenyezi Mungu mshirika katika kumuabudu. Kumpwekesha Mwenyezi Mungu huko, kwa kumhusu Yeye Peke Yake kwa ibada, ni miongoni mwa yale ambayo Mwenyezi Mungu Ametutunukia sisi na watu, lakini wengi zaidi wa watu hawamshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu na Imani.»
Faccirooji aarabeeji:
يَٰصَٰحِبَيِ ٱلسِّجۡنِ ءَأَرۡبَابٞ مُّتَفَرِّقُونَ خَيۡرٌ أَمِ ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ
Yūsuf akaendelea kusema kuwaambia vijana wawili waliokuwa na yeye jela, «Je, kuwaabudu waungu walioumbwa wa aina mbalimbali ni bora au ni kumuabudu Mwenyezi Mungu Aliye Mmoja, Mwenye kutendesha nguvu?
Faccirooji aarabeeji:
مَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِهِۦٓ إِلَّآ أَسۡمَآءٗ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِنِ ٱلۡحُكۡمُ إِلَّا لِلَّهِ أَمَرَ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّآ إِيَّاهُۚ ذَٰلِكَ ٱلدِّينُ ٱلۡقَيِّمُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ
«Nyinyi hamuabudu chochote kisichokuwa Mwenyezi Mungu isipokuwa ni majina yasiyokuwa na maana yoyote, mumeyafanya ni waola, nyinyi na baba zenu, kwa ujinga wenu na upotevu; Mwenyezi Mungu Hakuteremsha hoja au dalili yoyote juu ya usahihi wake. Hukumu ya haki ni ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Peke Yake, Asiye na mshirika. Yeye Ameamrisha kwamba msimwandame wala msimnyenyekee Asiyekuwa Yeye, na kwamba mumuabudu Yeye Peke Yake. Na hii ndiyo Dini iliyolingana sawa isiyokwenda kombo. Lakini wengi zaidi wa watu hawalielewi hilo, hawaujui uhakika wake.
Faccirooji aarabeeji:
يَٰصَٰحِبَيِ ٱلسِّجۡنِ أَمَّآ أَحَدُكُمَا فَيَسۡقِي رَبَّهُۥ خَمۡرٗاۖ وَأَمَّا ٱلۡأٓخَرُ فَيُصۡلَبُ فَتَأۡكُلُ ٱلطَّيۡرُ مِن رَّأۡسِهِۦۚ قُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ ٱلَّذِي فِيهِ تَسۡتَفۡتِيَانِ
«Enyi marafiki wangu gerezani, haya uchukueni uaguzi wa ndoto zenu: ama yule aliyeona kwenye ndoto yake kuwa anakamua zabibu, yeye atatoka jela na atakuwa ni mwenye kuishughulikia pombe ya mfalme. Ama mwingine aliyeota kuwa anabeba mkate juu ya kichwa chake, yeye atasulubiwa na aachwe, na ndege waje wamle kichwa chake. Limeshapitishwa jambo ambalo mlikuwa mnaliuliza na limeshamalizwa.»
Faccirooji aarabeeji:
وَقَالَ لِلَّذِي ظَنَّ أَنَّهُۥ نَاجٖ مِّنۡهُمَا ٱذۡكُرۡنِي عِندَ رَبِّكَ فَأَنسَىٰهُ ٱلشَّيۡطَٰنُ ذِكۡرَ رَبِّهِۦ فَلَبِثَ فِي ٱلسِّجۡنِ بِضۡعَ سِنِينَ
Hapo Yūsuf akamwambia yule aliyemjua kuwa ataokoka kati ya wale marafiki wake wawili, «Nitaje kwa bwanako mfalme na umwelezee kwamba mimi nimedhulumiwa, nimefungwa bila hatia.» Shetani akamsahaulisha mwanamume yule kumtajia mfalme hali ya Yūsuf, na kwa hivyo akakaa Yūsuf ndani ya jela myaka kadha.
Faccirooji aarabeeji:
وَقَالَ ٱلۡمَلِكُ إِنِّيٓ أَرَىٰ سَبۡعَ بَقَرَٰتٖ سِمَانٖ يَأۡكُلُهُنَّ سَبۡعٌ عِجَافٞ وَسَبۡعَ سُنۢبُلَٰتٍ خُضۡرٖ وَأُخَرَ يَابِسَٰتٖۖ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمَلَأُ أَفۡتُونِي فِي رُءۡيَٰيَ إِن كُنتُمۡ لِلرُّءۡيَا تَعۡبُرُونَ
Na mfalme akasema, «Mimi niliona ndotoni, katika kulala kwangu, ngombe saba wanono wanaliwa na ngombe saba walioambata kwa kukonda, na niliona visuke saba vibichi na visuke saba vikavu. Enyi mabwana na wakubwa, nipeni habari ya ndoto hii, iwapo nyinyi ndoto mnaagua.»
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore Yuusuf
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Eggo (nantino) ngo e Swahiliire - Abdullah Muhammad e Naasir Khamis. - Tippudi firooji ɗii

Eggi nde ko Dr. Abdalla Mohammed Abubakri e Seek Naasir Khamis.

Uddude