Check out the new design

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Eggo (nantino) ngo e Swahiliire - Abdullah Muhammad e Naasir Khamis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Simoore: Simoore koreeji imraan   Aaya:
ثُمَّ أَنزَلَ عَلَيۡكُم مِّنۢ بَعۡدِ ٱلۡغَمِّ أَمَنَةٗ نُّعَاسٗا يَغۡشَىٰ طَآئِفَةٗ مِّنكُمۡۖ وَطَآئِفَةٞ قَدۡ أَهَمَّتۡهُمۡ أَنفُسُهُمۡ يَظُنُّونَ بِٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ ظَنَّ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِۖ يَقُولُونَ هَل لَّنَا مِنَ ٱلۡأَمۡرِ مِن شَيۡءٖۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَمۡرَ كُلَّهُۥ لِلَّهِۗ يُخۡفُونَ فِيٓ أَنفُسِهِم مَّا لَا يُبۡدُونَ لَكَۖ يَقُولُونَ لَوۡ كَانَ لَنَا مِنَ ٱلۡأَمۡرِ شَيۡءٞ مَّا قُتِلۡنَا هَٰهُنَاۗ قُل لَّوۡ كُنتُمۡ فِي بُيُوتِكُمۡ لَبَرَزَ ٱلَّذِينَ كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقَتۡلُ إِلَىٰ مَضَاجِعِهِمۡۖ وَلِيَبۡتَلِيَ ٱللَّهُ مَا فِي صُدُورِكُمۡ وَلِيُمَحِّصَ مَا فِي قُلُوبِكُمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Kisha ikawa ni katika rehema ya Mwenyezi Mungu kwa waumini waliomtakasia nia kwamba Aliingiza kwenye nyoyo zao , baada ya kero na usumbufu uliowafika, utulivu na Imani thabiti kuhusu ahadi ya Mwenyezi Mungu kwao. Miongoni mwa alama za utulivu huo ni usingizi uliolifinika kundi katika wao, nalo ni lile la wale waliokuwa na ikhlasi na yakini kwa Mola wao. Na kundi lingine ilikuwa hamu ya watu wake ni kuziokoa nafsi zao; azma yao ilikuwa dhaifu, wakashughulishwa na nafsi zao na wakawa na dhana mbaya kwa Mola wao, kwa Dini Yake na kwa Mtume Wake.Wakadhani kwamba Mwenyezi Mungu Hatalitimiza jambo la Mtume Wake na kwamba Uislamu hautasimama ukaimarika. Kwa hivyo, utawaona ni wenye majuto juu ya kutoka kwao. Na huwa wakiambiana wao kwa wao, «Je tulikuwa na chaguo lolote katika kutoka kwetu kwenda kupigana?» Waambie, ewe Mtume, «Mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu. Yeye Ndiye Aliyepanga kutoka kwenu na (Ndiye Aliyepanga yale) yaliyowafikia.» Nao wanayaficha katika nafsi zao wasiyoyadhihirisha kwako ya majuto juu ya kutoka kwao kwenda mapiganoni. Huwa wakisema, «Lau kama tungalikuwa na hiyari japo ndogo, hatungeuawa hapa.» Waambie, «Ajali ziko mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Hata kama mlikuwa majumbani mwenu, na Mwenyezi Mungu Akakadiria mufe, wangalitoka wale ambao Mwenyezi Mungu Amewakadiria mauti, kwenda pale watakapouawa.» Na Hakuyafanya hayo Mwenyezi Mungu isipokuwa ni kuwapa nyinyi mtihani juu ya yaliyomo ndani ya vifua vyenu ya shaka na unafiki na ili Ampambanue mwema na maovu na lipate kudhihirika kwa watu jambo la Muumini na lile la mnafiki, la maneno na vitendo. Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa yaliyomo kwenye nyoyo za viumbe Wake. Hakuna chochote, katika mambo yao, kinachofichika Kwake.
Faccirooji aarabeeji:
إِنَّ ٱلَّذِينَ تَوَلَّوۡاْ مِنكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡتَقَى ٱلۡجَمۡعَانِ إِنَّمَا ٱسۡتَزَلَّهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ بِبَعۡضِ مَا كَسَبُواْۖ وَلَقَدۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Hakika wale waliokimbia kati yenu, enyi Maswahaba wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwenye vita siku waliokutana Waumimini na washirikina katika vita vya Uhud, ni Shetani ndiye aliyewatosa kwenye dhambi hili kutokana na baadhi ya madhambi waliyoyafanya. Kwa kweli Mwenyezi Mungu Amewasamehe na hakuwaadhibu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa Msamaha kwa wenye madhambi wanaotubia, ni Mpole Asiyekuwa na haraka ya kuwatesa wenye kumuasi.
Faccirooji aarabeeji:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَقَالُواْ لِإِخۡوَٰنِهِمۡ إِذَا ضَرَبُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ كَانُواْ غُزّٗى لَّوۡ كَانُواْ عِندَنَا مَا مَاتُواْ وَمَا قُتِلُواْ لِيَجۡعَلَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ حَسۡرَةٗ فِي قُلُوبِهِمۡۗ وَٱللَّهُ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo, msijifananishe na makafiri ambao hawamuamini Mola wao. Kwani wao huwaambia ndugu zao, miongoni mwa makafiri, wanapotoka kwenda kutafuta maisha yao katika ardhi au wanapokuwa pamoja na wapiganaji, wakafa au wakauawa, «Lau kama hawa hawangetoka wala hawangepigana na wakabakia pamoja na sisi, hawangekufa wala hawangeuawa.» Neno hili linawaongezea machungu, maudhiko na majuto yanayobakia katika nyoyo zao. Ama Waumini, wao wanajua kwamba hili limetokana na kadara ya Mwenyezi Mungu, ndipo Mwenyezi Mungu Huziongoza nyoyo zao na Huwasahilishia misiba. Na Mwenyezi Mungu Anambakisha hai yule Aliyemkadiria kuishi, hata kama ni msafiri au ni mpiganaji. Na Anamfisha yule ambaye muda wake wa kuishi umekoma, hata kama ni mkazi wa mji. Na Mwenyezi Mungu kwa kila mlifanyalo ni Mwenye kuliona, na Atawalipa kwalo.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَئِن قُتِلۡتُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوۡ مُتُّمۡ لَمَغۡفِرَةٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَحۡمَةٌ خَيۡرٞ مِّمَّا يَجۡمَعُونَ
Na iwapo mtauawa, enyi Waumini, katika hali ya kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu au mkafa vitani, Mwenyezi Mungu Atawasamehe madhmbi yenu na Atawarehemu rehema itokayo Kwake. Hapo mtafaulu kwa kuyapata mabustani ya Peponi yenye starehe nyingi. Hayo ni bora kuliko dunia na wanavyovikusanya wapenda dunia.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore koreeji imraan
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Eggo (nantino) ngo e Swahiliire - Abdullah Muhammad e Naasir Khamis. - Tippudi firooji ɗii

Eggi nde ko Dr. Abdalla Mohammed Abubakri e Seek Naasir Khamis.

Uddude