Check out the new design

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Eggo (nantino) ngo e Swahiliire - Abdullah Muhammad e Naasir Khamis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Simoore: Simoore koreeji imraan   Aaya:
وَلِيُمَحِّصَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَيَمۡحَقَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na kushindwa huku kuliotokea katika vita vya Uhud kulikuwa ni kuwafanyia mtihani, kuwasafisha Waumini, kuwatakasa na wanafiki na ni maangamivu kwa makafiri.
Faccirooji aarabeeji:
أَمۡ حَسِبۡتُمۡ أَن تَدۡخُلُواْ ٱلۡجَنَّةَ وَلَمَّا يَعۡلَمِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ جَٰهَدُواْ مِنكُمۡ وَيَعۡلَمَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Enyi Maswahaba wa Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie! Kwani mnadhani kwamba mtaingia Peponi na bado hamjapewa mitihani ya vita na mambo mazito? Haitapatikana kwenu kuingia Peponi tu, hivi hivi, mpaka mjaribiwe na Awajuwe Mwenyezi Mungu, ujuzi ulio wazi kwa viumbe, wale wapiganao jihadi kati yenu katika njia Yake na wenye subira ya kupambana na maadui.
Faccirooji aarabeeji:
وَلَقَدۡ كُنتُمۡ تَمَنَّوۡنَ ٱلۡمَوۡتَ مِن قَبۡلِ أَن تَلۡقَوۡهُ فَقَدۡ رَأَيۡتُمُوهُ وَأَنتُمۡ تَنظُرُونَ
Na kwa hakika mlikuwa, enyi Waumini, kabla ya vita vya Uhud mnatamani kukutana na maadui zenu, ili mpate utukufu wa jihadi na kufa mashahidi katika njia ya Mwenyezi Mungu ambao walibahatika nao ndugu zenu kwenye vita vya Badr. Basi hilo ndilo, Iimeshapatikana kwenu, mlilolitamani na mkaliomba. Basi jitokezeni mpigane na msubirishane.
Faccirooji aarabeeji:
وَمَا مُحَمَّدٌ إِلَّا رَسُولٞ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِ ٱلرُّسُلُۚ أَفَإِيْن مَّاتَ أَوۡ قُتِلَ ٱنقَلَبۡتُمۡ عَلَىٰٓ أَعۡقَٰبِكُمۡۚ وَمَن يَنقَلِبۡ عَلَىٰ عَقِبَيۡهِ فَلَن يَضُرَّ ٱللَّهَ شَيۡـٔٗاۚ وَسَيَجۡزِي ٱللَّهُ ٱلشَّٰكِرِينَ
Hakuwa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni kiumbe aina nyingine, isipokuwa yeye ni Mtume wa jinsi ya Mitume wengine waliokuweko kabla yake, afikisha ujumbe wa Mola wake. Basi iwapo atakufa, kwa kumalizika muda wake, au atauawa, kama walivyoeneza uvumi maadui, kwani mtarudi nyuma na kuacha dini yenu na kuyaacha aliyowaletea Mtume wenu? Basi yoyote miongoni mwenu atakayerudi nyuma akaiacha dini yake, yeye hatamdhuru Mwenyezi Mungu chochote, bali ataidhuru nafsi yake madhara makubwa. Ama atakayekuwa na msimamo imara juu ya Imani yake na akamshukuru Mola wake juu ya neema ya Uislamu, hakika Mwenyezi Mungu Atamlipa malipo mazuri kabisa.
Faccirooji aarabeeji:
وَمَا كَانَ لِنَفۡسٍ أَن تَمُوتَ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِ كِتَٰبٗا مُّؤَجَّلٗاۗ وَمَن يُرِدۡ ثَوَابَ ٱلدُّنۡيَا نُؤۡتِهِۦ مِنۡهَا وَمَن يُرِدۡ ثَوَابَ ٱلۡأٓخِرَةِ نُؤۡتِهِۦ مِنۡهَاۚ وَسَنَجۡزِي ٱلشَّٰكِرِينَ
Hakuna yoyote atakayekufa isipokuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na makadirio Yake na mpaka aufikishe muda ambao Mwenyezi Mungu Amempangia. Hayo ni maandishi yaliyopangiwa wakati. Na yoyote ambaye kwa vitendo vyake anataka manufaa ya duniani, tutampa tulichomgawia cha riziki, na hatakuwa na fungu lolote kesho Akhera. Na yoyote ambaye anataka kwa vitendo vyake malipo ya Mwenyezi Mungu huko Akhera , tutampa kile alichokitaka na tutampa malipo yake kamili pamoja na fungu lake duniani la riziki alilogawiwa. Kwani huyu kwa utiifu wake na jihadi yake ametushukuru; na wenye kushukuru tutawalipa mema.
Faccirooji aarabeeji:
وَكَأَيِّن مِّن نَّبِيّٖ قَٰتَلَ مَعَهُۥ رِبِّيُّونَ كَثِيرٞ فَمَا وَهَنُواْ لِمَآ أَصَابَهُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَمَا ضَعُفُواْ وَمَا ٱسۡتَكَانُواْۗ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلصَّٰبِرِينَ
Wengi kati ya Mitume waliotangulia, walipigana pamoja nao makundi mengi ya watu waliowafuata. Hawakudhoofika kwa yale yaliyowapata ya majaraha au mauaji, kwani hayo yalikuwa katika njia ya Mola wao. Wala hawakulemewa wala hawakumnyenyekea adui yao, bali walisubiri kwa yaliyowapata. Na Mwenyezi Mungu Anawapenda wenye kusubiri.
Faccirooji aarabeeji:
وَمَا كَانَ قَوۡلَهُمۡ إِلَّآ أَن قَالُواْ رَبَّنَا ٱغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَا وَإِسۡرَافَنَا فِيٓ أَمۡرِنَا وَثَبِّتۡ أَقۡدَامَنَا وَٱنصُرۡنَا عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na halikuwa neno la hawa wenye kusubiri isipokuwa ni kusema, «Ewe Mola wetu! Tusamehe madhambi yetu na yaliyotokea kwetu ya kuruka mipaka katika mambo ya dini yetu na uzithibitishe nyayo zetu, tusipate kukimbia tunapopigana na adui yetu na utunusuru na yule anayepinga umoja wako na unabii wa Manabii wako.
Faccirooji aarabeeji:
فَـَٔاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ ثَوَابَ ٱلدُّنۡيَا وَحُسۡنَ ثَوَابِ ٱلۡأٓخِرَةِۗ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Basi Aliwapa Mwenyezi Mungu, wale wenye kusubiri, malipo yao duniani kwa kuwanusuru na maadui zao, kwa kuwafanya wakae kwa utulivu katika ardhi na kwa malipo mema yaliyo makubwa Akhera, nayo ni mabustani ya Peponi yaliyojaa neema. Na Mwenyezi Mungu Anampenda kila mtenda wema katika kumuabudu Mola wake na kuamiliana kwake na viumbe Wake.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore koreeji imraan
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Eggo (nantino) ngo e Swahiliire - Abdullah Muhammad e Naasir Khamis. - Tippudi firooji ɗii

Eggi nde ko Dr. Abdalla Mohammed Abubakri e Seek Naasir Khamis.

Uddude