Ewe Nabii! Waambie mateka waliomo mikononi mwenu: Kama Mwenyezi akiona kheri yoyote nyoyoni mwenu atakupeni bora kuliko vilivyo chukuliwa kwenu, na atakusameheni. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Ewe Nabii! Waambie hao mateka walio angukia mikononi mwenu: Ikiwa katika nyoyo zenu ipo kheri anayo ijua Mwenyezi Mungu, Yeye atakulipeni yaliyo bora zaidi kuliko hicho walicho kichukua Waumini, na atakusameheni ushirikina wenu na madhambi mliyo kuwa nayo. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghfira na rehema kwa mwenye kutubia madhambi yake.
Ikiwa wanataka kukufanyia khiana, wao walikwisha mfanyia khiana Mwenyezi Mungu kabla yake, na Yeye akakuwezesha kuwashinda. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye hikima.
Na pindi wakitaka kukukhuni, kwa vile baadhi yao walivyo onyesha kumili kwenye Uislamu, pamoja na nyoyo zao kupenda kukufanyia khiana makusudi, wewe usivunjike moyo. Mwenyezi Mungu atakupa uwezo juu yao. Kama hapo kwanza walipo mkhini Mwenyezi Mungu kwa kumfanyia wenzi na washirika wa kuwaabudu, na wakaikufuru neema yake, na Yeye aliwaweza kwa kukupa ushindi juu yao katika Badri, juu ya kuwa jeshi lako ni dogo na lao ni kubwa. Na Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye ushindi, Muendeshaji kwa hikima yake, aliwathibitisha wakawa na nguvu waja wake Waumini kwa nusura yake.
Hakika wale walio amini na wakahama na wakapigania Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao, na wale walio toa mahala pa kukaa, na wakanusuru, hao ni marafiki na walinzi wao kwa wao. Na wale walio amini lakini hawakuhama, nyinyi hamna waajibu wa ulinzi kwao hata kidogo mpaka wahame. Lakini wakiomba msaada kwenu katika Dini, basi ni juu yenu kuwasaidia, isipo kuwa juu ya watu ambao yapo mapatano baina yenu na wao. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayo yatenda.
Hakika walio isadiki Haki na wakaikubali hukumu yake, wakahama Makka, wakapigana Jihadi kwa mali yao na roho zao, na wale walio wapa makaazi wakimbizi ugenini, wakamsaidia Mtume wa Mwenyezi Mungu, wanapigana vita na wale wanao wapiga vita. Wanamfanyia uadui anao wafanyia uadui. Wao kwa wao wanasaidia kuunga mkono Haki, na kutukuza Neno la Mwenyezi Mungu. Na wale wasio hama, haijathibiti kupata ulinzi na msaada wa Waumini, mpaka wahajiri. Lakini wakikutakeni muwanusuru na wanao wakandamiza katika Dini, basi wanusuruni. Wakikutakeni muwasaidie dhidi ya watu ambao mna mapatano nao, na wala hawakuvunja mapatano hayo, basi msiwakubalie. Na Mwenyezi Mungu anayaona myatendayo, hana kinacho fichika kwake. Basi simameni kwenye mipaka yake msije mkatumbukia katika adhabu yake.
Na wale walio kufuru ni marafiki wenyewe kwa wenyewe. Msipo fanya hivi itakuwako fitna katika nchi na fisadi kubwa.
Na walio kufuru wao ni marafiki wenyewe kwa wenyewe. Na wao husaidiana kwa mambo ya upotovu, na wanaungana mkono kukufanyieni nyinyi uadui. Basi nyinyi msifanye nao urafiki. Mkikhaalifu, yaani mkenda kinyume na haya mkawafanya ni wenzenu itaingia fitna katika safu zenu, na utakuwa uharibifu mkubwa katika nchi.
Na walio amini wakahama na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na walio toa mahala pa kukaa na wakanusuru, hao ndio Waumini wa kweli. Watapata msamaha wa Mwenyezi Mungu na kuruzukiwa kwema.
Na walio amini, na wakahajiri, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na walio wapa makaazi, na wakaisaidia Haki na Neno la Mwenyezi Mungu - hao ndio walio na Imani ya kweli. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu atawasamehe, na watapata riziki kubwa duniani na Akhera.
Na watakao amini baadaye na wakahajiri, na wakapigana Jihadi pamoja nanyi, basi hao ni katika nyinyi. Na jamaa wa nasaba wanastahikiana wenyewe kwa wenyewe zaidi katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua kila kitu.
Na walio amini baada ya wale wa mwanzo, na mwishoe wakahama nao, na wakapigana Jihadi pamoja na walio tangulia, basi hao ni katika nyinyi, kwa mkusanyiko wa Muhaajirina (Walio hama Makka) na Ansari (walio msaidia Mtume, watu wa Madina). Hao wanastahiki ulinzi na haki kama ziliopo baina ya nyinyi kwa nyinyi. Na walio kuwa wame nasibiana katika Waumini - juu ya urafiki wa Imani -wana urafiki zaidi wa kuwa ni jamaa. Basi hao wanazidiana katika mapenzi, na mali, na kusaidiana, na kuungana mkono. Na Mwenyezi Mungu ameyabainisha hayo katika Kitabu chake. Naye ni Mwenye kujua kila kitu.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
સંશોધનના પરિણામો:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".