Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Aya: (27) Sura: Ibrahim
يُثَبِّتُ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱلۡقَوۡلِ ٱلثَّابِتِ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِۖ وَيُضِلُّ ٱللَّهُ ٱلظَّٰلِمِينَۚ وَيَفۡعَلُ ٱللَّهُ مَا يَشَآءُ
Mwenyezi Mungu Anawathibitisha wale waloamini kwenye neno la ukweli lenye uimara nalo ni kukubali kwamba hakuna mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwamba Muhaamad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwamba Atawathibitisha kwenye dini ya kweli aliyokuja nayo katika huu ulimwengu, Atawapa mwisho mwema wakati wa kufa, na Atawaongoza watoe jawabu ya sawa watakapoulizwa na Malaika wawili kaburini. Na Mwenyezi Mungu Atawapoteza madhalimu wasiuone usawa ulimenguni na Akhera. Na Mwenyezi Mungu Anafanya Analolitaka kwa kuwaafikia wenye kuamini na kutowaongoza wenye kukufuru na kuasi.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (27) Sura: Ibrahim
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Dr. Abdullahi Muhammad Abubakar da Sheikh Nasir Khamis suka fassarata.

Rufewa