Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Aya: (259) Sura: Suratu Al'bakara
أَوۡ كَٱلَّذِي مَرَّ عَلَىٰ قَرۡيَةٖ وَهِيَ خَاوِيَةٌ عَلَىٰ عُرُوشِهَا قَالَ أَنَّىٰ يُحۡيِۦ هَٰذِهِ ٱللَّهُ بَعۡدَ مَوۡتِهَاۖ فَأَمَاتَهُ ٱللَّهُ مِاْئَةَ عَامٖ ثُمَّ بَعَثَهُۥۖ قَالَ كَمۡ لَبِثۡتَۖ قَالَ لَبِثۡتُ يَوۡمًا أَوۡ بَعۡضَ يَوۡمٖۖ قَالَ بَل لَّبِثۡتَ مِاْئَةَ عَامٖ فَٱنظُرۡ إِلَىٰ طَعَامِكَ وَشَرَابِكَ لَمۡ يَتَسَنَّهۡۖ وَٱنظُرۡ إِلَىٰ حِمَارِكَ وَلِنَجۡعَلَكَ ءَايَةٗ لِّلنَّاسِۖ وَٱنظُرۡ إِلَى ٱلۡعِظَامِ كَيۡفَ نُنشِزُهَا ثُمَّ نَكۡسُوهَا لَحۡمٗاۚ فَلَمَّا تَبَيَّنَ لَهُۥ قَالَ أَعۡلَمُ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Au je uliona, ewe Mtume, mfano wa yule aliyepita kwenye kijiji ambacho nyumba zake zilikuwa zimevunjika na kuangukia misingi yake na akasema, «Vipi Mwenyezi Mungu Atakihuisha kijiji hiki baada ya kuwa kimekufa?» Mwenyezi Mungu Akamfisha miaka mia moja kisha Akamrudishia roho yake na Akamwambia, «Ni kwa muda gani ulikuwa umekufa?» Akasema, «Nilikuwa nimekufa kwa muda wa siku moja au sehemu ya siku.» Akampa habari kuwa alikuwa amekufa kwa muda wa miaka mia. Na Akamuamrisha akiangalie chakula chake na kinywaji chake vipi Mwenyezi Mungu Amevihifadhi visiharibike muda huu mrefu. Na Akamuamrisha amtazame punda wake aone vipi Mwenyezi Mungu Alimuhuisha baada ya kuwa mifupa iliyotapakaa. Na Akamwambia, «Na ili tukufanye wewe ni dalili kwa watu.» Yaani: dalili iliyo wazi ya uweza wa Mwenyezi Mungu kufufua baada ya kufa. Na akamuamrisha aitazame mifupa aone vipi Mwenyezi Mungu Anavyoiinua baadhi yake juu ya mingine na kuiunganisha baadhi yake na mingine na kuivisha nyama baada ya kushikana na kisha kuirudishia uhai.Yalipomfunukia hayo waziwazi alikubali ukubwa wa Mwenyezi Mungu na kuwa Yeye ni Muweza wa kila kitu. Na akawa ni dalili kwa watu.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (259) Sura: Suratu Al'bakara
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Rufewa