Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Aya: (176) Sura: Suratu Al'nisaa
يَسۡتَفۡتُونَكَ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِي ٱلۡكَلَٰلَةِۚ إِنِ ٱمۡرُؤٌاْ هَلَكَ لَيۡسَ لَهُۥ وَلَدٞ وَلَهُۥٓ أُخۡتٞ فَلَهَا نِصۡفُ مَا تَرَكَۚ وَهُوَ يَرِثُهَآ إِن لَّمۡ يَكُن لَّهَا وَلَدٞۚ فَإِن كَانَتَا ٱثۡنَتَيۡنِ فَلَهُمَا ٱلثُّلُثَانِ مِمَّا تَرَكَۚ وَإِن كَانُوٓاْ إِخۡوَةٗ رِّجَالٗا وَنِسَآءٗ فَلِلذَّكَرِ مِثۡلُ حَظِّ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۗ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمۡ أَن تَضِلُّواْۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمُۢ
Wanakuuliza, ewe Nabii, kuhusu hukumu ya urithi wa kalalah, naye ni aliyekufa akiwa hana mwana wala mzazi. Sema, «Mwenyezi Mungu Anawafafanulia hukumu yake, kwamba yoyote atakayefariki na akawa hana mwana wala mzazi, na akawa ana dada yake wa kwa baba na mama au wa kwa baba tu. Basi dada huyo atapata nusu ya mali yaliyoachwa na aliyefariki. Na iwapo aliyefariki ni huyo dada, na akawa hana mwana wala mzazi, basi kaka yake, wa kwa baba na mama au wa kwa baba, atarithi mali yote. Na iwapo yule aliyefariki, bila ya kuacha mwana wala mzazi, ana dada zake wawili, basi wao watapata theluthi mbili ya mali aliyoyaacha. Na watakapokusanyika pamoja kwenye urithi ndugu wa kiume na wa kike wasiokuwa wa kwa mama basi kila mmoja, katika ndugu wa kiume, atapata mfano wa mafungu mawili ya mwanamke. Mwenyezi Mungu Anawafafanulia namna ya kugawanya urithi na hukumu ya aliyefariki bila ya kuacha mwana wala mzazi, ili msije mkapotea kwenye njia ya haki kuhusu hukumu ya mambo ya uraihi. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzu wa mwisho wa mambo na yaliyo na heri kwa waja Wake.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (176) Sura: Suratu Al'nisaa
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da yaren Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Rufewa