Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Al'ahkab   Aya:
وَإِذَا حُشِرَ ٱلنَّاسُ كَانُواْ لَهُمۡ أَعۡدَآءٗ وَكَانُواْ بِعِبَادَتِهِمۡ كَٰفِرِينَ
Na pindi watu watakapokusanywa Siku ya Kiyama ili wahesabiwe na walipwe, wale waungu waliokuwa wakiwaomba duniani watakuwa ni maadui zao, wakiwalaani na kujiepusha nao na kukanusha kuwa wao walikuwa wanajua kuwa wale wanawaabudu wao.
Tafsiran larabci:
وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُنَا بَيِّنَٰتٖ قَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ هَٰذَا سِحۡرٞ مُّبِينٌ
Na washirikina wanaposomewa aya zetu zilizobainishwa waziwazi, wanasema hao makafiri wakati ule Qur’ani inapowajia, “Huu ni uchawi waziwazi.”
Tafsiran larabci:
أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ إِنِ ٱفۡتَرَيۡتُهُۥ فَلَا تَمۡلِكُونَ لِي مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـًٔاۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَا تُفِيضُونَ فِيهِۚ كَفَىٰ بِهِۦ شَهِيدَۢا بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۖ وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
Au je wanasema hawa washirikina kwamba Muhammad ameizua Qur’ani? Waambie, ewe mtume, “Iwapo mimi nimemzulia Mwenyezi Mungu hii Qur’ani, basi nyinyi hamuwezi kunikinga mimi na adhabu ya Mwenyezi Mungu kitu chochote Akiwa atanitesa kwa hilo. Yeye, kutakasika ni Kwake, ni Mjuzi zaidi wa kile mnachokisema juu ya hii Qur’ani kuliko kitu chochote kingine. Inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni Shahidi juu yangu mimi na nyinyi, na Yeye Ndiye Mwingi wa msamaha kwa waja Wake, ni Mwingi wa rehema kwa waja Wake Waumini.”
Tafsiran larabci:
قُلۡ مَا كُنتُ بِدۡعٗا مِّنَ ٱلرُّسُلِ وَمَآ أَدۡرِي مَا يُفۡعَلُ بِي وَلَا بِكُمۡۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّ وَمَآ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Sema, ewe Mtume, uwambie washirikina wa watu wako, “Sikuwa ni wa mwnzo wa wajumbe wa Mwenyezi Mungu kwa viumbe Wake. Na sijui Atakalofanya Mwenyezi Mngu kwangu wala kwenu hapa duniani. Sifuati katika yale ninayowaamrisha nyinyi na katika yale ninayoyafanya isipokuwa wahyi wa Mwenyezi Mungu Anaoniletea mimi. Na sikuwa mimi isipokuwa ni mwenye kuonya ambaye uonyaji wake uko wazi.»
Tafsiran larabci:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كَانَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ وَكَفَرۡتُم بِهِۦ وَشَهِدَ شَاهِدٞ مِّنۢ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ عَلَىٰ مِثۡلِهِۦ فَـَٔامَنَ وَٱسۡتَكۡبَرۡتُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Sema , ewe Mtume, uwaambie washirikina wa watu wako, “Nipasheni habari: ikiwa hii Qur’ani inatoka kwa Mwenyezi Mungu na mkaikanusha, na hali ameshuhudia shahidi kati ya Wana wa Isrāīl, kama ‘Abdullāh bin Salām, kwa mfano wa hii Qur’ani, nayo ni yaliyomo ndani ya Taurati ya kusadikisha unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, akaiamini na akayafuata kivitendo yaliyokuja ndani ya Qur’ani, na nyinyi mkakanusha hilo kwa njia ya kiburi. Basi ni upi huu isipokuwa ni udhalimu mkubwa na ukafiri mwingi?” Hakika Mwenyezi Mungu Hawaongozi kwenye Uislamu na kuifikia haki wale watu waliojidhulumu kwa kumkanusha Mwenyezi Mungu.
Tafsiran larabci:
وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَوۡ كَانَ خَيۡرٗا مَّا سَبَقُونَآ إِلَيۡهِۚ وَإِذۡ لَمۡ يَهۡتَدُواْ بِهِۦ فَسَيَقُولُونَ هَٰذَآ إِفۡكٞ قَدِيمٞ
Na wale walioukanusha unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, walisema wakiwaambia wale waliomuamini, “Lau huko kumuamini Muhammad kwa aliyokuja nayo ni kheri hamngalitutangulia kuamini.” Na kwa kuwa hawakujiongoza na hii Qur’ani wala hawakunufaika na ukweli uliyomo ndani yake, watasema, “Huu ni urongo uliopokewa kwa watu wa kale.”
Tafsiran larabci:
وَمِن قَبۡلِهِۦ كِتَٰبُ مُوسَىٰٓ إِمَامٗا وَرَحۡمَةٗۚ وَهَٰذَا كِتَٰبٞ مُّصَدِّقٞ لِّسَانًا عَرَبِيّٗا لِّيُنذِرَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُحۡسِنِينَ
Na kabla ya hii Qur’ani, tuliiteremsha Taurati ikiwa ni muongozo kwa Wana wa Isrāīl waiandame na ni rehema kwa wenye kuiamini na kuifuata kivitendo. Na hii Qur’ani inasadikisha Vitabu vilivyokuwa kabla yake. Tumeiteremsha kwa lugha ya Kiarabu ili iwaonye wale waliozidhulumu nafsi zao kwa kukanusha na kuasi. Na bishara njema ni ya wale waliomtii Mwenyezi Mungu na wakafanya wema katika Imani yao na utiifu wao duniani.
Tafsiran larabci:
إِنَّ ٱلَّذِينَ قَالُواْ رَبُّنَا ٱللَّهُ ثُمَّ ٱسۡتَقَٰمُواْ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Hakika wale waliosema, “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu” kisha wakalingana sawa katika kumuamini, basi hao hawatakuwa na khofu ya babaiko la Siku ya Kiyama na vituko vyake, wala hawatasikitka juu ya hadhi za duniani walizoziacha nyuma yao
Tafsiran larabci:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِ خَٰلِدِينَ فِيهَا جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Hao ni wa watu wa Peponi, watakaa humo milele kwa rehema za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, juu yao , na kwa yale waliyoyatanguliza ya matendo mema katika dunia yao.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'ahkab
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Dr. Abdullahi Muhammad Abubakar da Sheikh Nasir Khamis suka fassarata.

Rufewa