Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Al'mulk   Aya:

Al-Mulk

تَبَٰرَكَ ٱلَّذِي بِيَدِهِ ٱلۡمُلۡكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ
Zimekithiri kheri za Mwenyezi Mungu na wema Wake kwa viumbe Vyake, Ambaye mkononi Mwake upo ufalme wa duniani na Akhera na mamlaka ya viwili hivyo, Anapitisha amri Yake na uamuzi Wake kwenye mamlaka Yake hayo, na Yeye kwa kila jambo ni Muweza. Faida inayopatikana katika aya hii ni kuwa inathibitisha sifa ya mkono kwa Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, kwa namna inavyonasibiana na utukufu Wake.
Tafsiran larabci:
ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلۡمَوۡتَ وَٱلۡحَيَوٰةَ لِيَبۡلُوَكُمۡ أَيُّكُمۡ أَحۡسَنُ عَمَلٗاۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفُورُ
Aliyeumba mauti na uhai ili awatahini nyinyi, enyi watu, ni yupi miongoni mwenu aliye mwema wa matendo na utakasaji wa nia? Na Yeye Ndiye Mshindi Ambaye hakuna chochote kinachomshinda, Ndiye Mwingi wa msamaha kwa anayetubia miongonu mwa waja Wake. Katika aya hii pana kuhimiza kufanya utiifu na makaemeo ya kutenda maasia.
Tafsiran larabci:
ٱلَّذِي خَلَقَ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖ طِبَاقٗاۖ مَّا تَرَىٰ فِي خَلۡقِ ٱلرَّحۡمَٰنِ مِن تَفَٰوُتٖۖ فَٱرۡجِعِ ٱلۡبَصَرَ هَلۡ تَرَىٰ مِن فُطُورٖ
Aliyeumba mbingu saba zilizopangika, baadahi yake juu ya nyingine, huoni katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema, ewe mwenye kuangalia, tofauti yoyote wala mpambanuko, basi rudia tena kuangalia mbinguni: je unaona pasuko zozote au nyufa?
Tafsiran larabci:
ثُمَّ ٱرۡجِعِ ٱلۡبَصَرَ كَرَّتَيۡنِ يَنقَلِبۡ إِلَيۡكَ ٱلۡبَصَرُ خَاسِئٗا وَهُوَ حَسِيرٞ
Kisha rudia kuangalia tena, mara baada ya mara, yatakurudia hayo macho yakiwa manyonge na matwevu hayakuona upungufu wowote na hali yakiwa ni yenye usumbufu na uchovu.
Tafsiran larabci:
وَلَقَدۡ زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِمَصَٰبِيحَ وَجَعَلۡنَٰهَا رُجُومٗا لِّلشَّيَٰطِينِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابَ ٱلسَّعِيرِ
Na hakika tumeupamba uwingu wa karibu unaoonekana na macho kwa nyota kubwa zenye kung’ara, na tumezifanya nyota hizo ni vimondo zenye kuwachoma wenye kusikiliza kwa kuiba miongoni mwa mashetani, na tumewaandalia wao huko Akhera adhabu ya Moto wenye kuwaka wakawa ni wenye kuadhibika kwa joto lake.
Tafsiran larabci:
وَلِلَّذِينَ كَفَرُواْ بِرَبِّهِمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Na wenye kumkanusha Mola wao watapata adhabu ya moto wa Jahanamu, na ubaya zaidi wa mahali pa mtu kurejea ni ni huo moto wa Jahanamu!
Tafsiran larabci:
إِذَآ أُلۡقُواْ فِيهَا سَمِعُواْ لَهَا شَهِيقٗا وَهِيَ تَفُورُ
Waingizwapo hao wakanushaji ndani ya moto wa Jahanamu, watausikia ukitoa sauti kali yenye kutisha , huku ukichemka machemko makali sana.
Tafsiran larabci:
تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ ٱلۡغَيۡظِۖ كُلَّمَآ أُلۡقِيَ فِيهَا فَوۡجٞ سَأَلَهُمۡ خَزَنَتُهَآ أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَذِيرٞ
unakaribia huo moto wa Jahanamu kurarukararuka kwa ukali wa hasira ulizonazo juu ya wakanushaji. Kila linapotiwa humo kundi la watu, wale wawakilishi wa kusimamia mambo ya huo moto wa Jahanamu watawauliza kwa njia ya kuwalaumu na kuwakaripia: Je kwani hakuwajia nyinyi, huko duniani, mjumbe wa kuwatahadharisha na adhabu hii ambayo nyinyi mmo ndani yake?
Tafsiran larabci:
قَالُواْ بَلَىٰ قَدۡ جَآءَنَا نَذِيرٞ فَكَذَّبۡنَا وَقُلۡنَا مَا نَزَّلَ ٱللَّهُ مِن شَيۡءٍ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا فِي ضَلَٰلٖ كَبِيرٖ
Watawajibu kwa kusema, «Ndio! Tumejiwa na Mjumbe anayetoka kwa Mwenyezi mungu akatuonya na tukamkanusha na tukasema kuhusu miujiza aliyokuja nayo: Mwenyezi Mungu hakumteremshia binadamu kitu chochote. Hamkuwa nyinyi, enyi Mitume, isipokuwa mmeenda mbali na haki.
Tafsiran larabci:
وَقَالُواْ لَوۡ كُنَّا نَسۡمَعُ أَوۡ نَعۡقِلُ مَا كُنَّا فِيٓ أَصۡحَٰبِ ٱلسَّعِيرِ
Na watasema kwa kukubali makosa, «Lau tungalikuwa tunasikia usikivu wa mwenye kutafuta haki, au tunafikiria juu ya yale tunayoitiwa kwayo, hatungekuwa ni kati ya watu wa Motoni.»
Tafsiran larabci:
فَٱعۡتَرَفُواْ بِذَنۢبِهِمۡ فَسُحۡقٗا لِّأَصۡحَٰبِ ٱلسَّعِيرِ
Hivyo basi wakakubali kukanusha kwao na kukufuru kwao kulikowafanya wastahili adhabu ya Moto. Basi kuwa mbali na rehema ya Mwenyezi Mungu ni kwa watu wa Motoni!
Tafsiran larabci:
إِنَّ ٱلَّذِينَ يَخۡشَوۡنَ رَبَّهُم بِٱلۡغَيۡبِ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٞ كَبِيرٞ
Hakika wale wanaomuogopa Mola wao, wakamuabudu na wasimuasim na hali wako mbali na macho ya watu na wanaiogopa adhabu ya Akhera kabla hawajaiona, watapata msamaha wa dambi zao katoka kwa Mwenyezi Mungu na malipo mema makubwa ambayo ni Pepo.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'mulk
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Dr. Abdullahi Muhammad Abubakar da Sheikh Nasir Khamis suka fassarata.

Rufewa