Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Aya: (72) Sura: Al'anfal
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَٱلَّذِينَ ءَاوَواْ وَّنَصَرُوٓاْ أُوْلَٰٓئِكَ بَعۡضُهُمۡ أَوۡلِيَآءُ بَعۡضٖۚ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَمۡ يُهَاجِرُواْ مَا لَكُم مِّن وَلَٰيَتِهِم مِّن شَيۡءٍ حَتَّىٰ يُهَاجِرُواْۚ وَإِنِ ٱسۡتَنصَرُوكُمۡ فِي ٱلدِّينِ فَعَلَيۡكُمُ ٱلنَّصۡرُ إِلَّا عَلَىٰ قَوۡمِۭ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُم مِّيثَٰقٞۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ
Hakika wale ambao wamemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakazifuata sheria Zake kivitendo, wakahama kwenda kwenye Nyumba ya Uislamu au nchi ambayo wataweza hapo kumuabudu Mola wao, wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali na nafsi, na Wale ambao waliowaweka Wahamiaji katika nyumba zao, wakawaliwaza kwa mali yao nawakaitetea dini ya Mwenyezi Mungu, hao ni wenye kusaidiana wao kwa wao. Ama wale walioamini na wasigure kutoka kwenye Nyumba ya ukafiri, basi nyinyi hamlazimishwi kuwahami na kuwatetea mpaka watakapogura. Na wakifanyiwa maonevu na Makafiri na wakataka msaada wenu, basi wakubalieni, isipokuwa iwapo ni dhidi ya watu ambao kuna makubaliano ya mkazo baina yenu na wao na hawajayavunja. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona matendo yenu, Atamlipa kila mtu kwa kadiri ya nia yake na tendo lake.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Aya: (72) Sura: Al'anfal
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassara da harshen Sawahili - Abdullah Muhammad da Nasir Khamis - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Dr. Abdullahi Muhammad Abubakar da Sheikh Nasir Khamis suka fassarata.

Rufewa