Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Al'nisaa   Aya:
فَبِمَا نَقۡضِهِم مِّيثَٰقَهُمۡ وَكُفۡرِهِم بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَقَتۡلِهِمُ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَقَوۡلِهِمۡ قُلُوبُنَا غُلۡفُۢۚ بَلۡ طَبَعَ ٱللَّهُ عَلَيۡهَا بِكُفۡرِهِمۡ فَلَا يُؤۡمِنُونَ إِلَّا قَلِيلٗا
Basi kwa sababu ya kuvunja kwao agano zao, na kuzikufuru kwao ishara za Mwenyezi Mungu, na kuwauwa kwao Manabii bila ya haki, na kusema kwao: 'Nyoyo zetu zimefumbwa'; bali Mwenyezi Mungu ameziziba kwa kufuru zao, basi hawaamini isipokuwa kidogo tu.
Tafsiran larabci:
وَبِكُفۡرِهِمۡ وَقَوۡلِهِمۡ عَلَىٰ مَرۡيَمَ بُهۡتَٰنًا عَظِيمٗا
Na kwa kufuru zao na kusema kwao juu ya Maryam uongo mkubwa.
Tafsiran larabci:
وَقَوۡلِهِمۡ إِنَّا قَتَلۡنَا ٱلۡمَسِيحَ عِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ رَسُولَ ٱللَّهِ وَمَا قَتَلُوهُ وَمَا صَلَبُوهُ وَلَٰكِن شُبِّهَ لَهُمۡۚ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ لَفِي شَكّٖ مِّنۡهُۚ مَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍ إِلَّا ٱتِّبَاعَ ٱلظَّنِّۚ وَمَا قَتَلُوهُ يَقِينَۢا
Na kusema kwao: 'Hakika, sisi tulimuua Masihi Isa, mwana wa Maryam, Mtume wa Mwenyezi Mungu.' Nao hawakumuua wala hawakumsulubisha, bali walifananishiwa tu. Na hakika wale waliohitilafiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana elimu yoyote nayo isipokuwa ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuua kwa yakini.
Tafsiran larabci:
بَل رَّفَعَهُ ٱللَّهُ إِلَيۡهِۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَزِيزًا حَكِيمٗا
Bali Mwenyezi Mungu alimwinua kwenda kwake, na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima.
Tafsiran larabci:
وَإِن مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ إِلَّا لَيُؤۡمِنَنَّ بِهِۦ قَبۡلَ مَوۡتِهِۦۖ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكُونُ عَلَيۡهِمۡ شَهِيدٗا
Na hawi katika Watu wa Kitabu isipokuwa hakika atamuamini yeye kabla ya kufa kwake. Naye Siku ya Kiyama atakuwa shahidi juu yao.[1]
[1] Hakuna hata mmoja katika Watu wa Kitabu (Mayahudi na Wakristo) ambaye hatamwamini Isa, amani iwe juu yake, baada ya kuteremka kwake katika mwisho wa zama na kabla ya kufa kwake Isa katika zama hizo. Na Siku ya Kiyama, Isa, amani iwe juu yake, atakuwa shahidi juu ya matendo yao. Yale yanayokubaliana na sheria na yale yanayopingana nayo. (Tafsir Assa'adiy)
Tafsiran larabci:
فَبِظُلۡمٖ مِّنَ ٱلَّذِينَ هَادُواْ حَرَّمۡنَا عَلَيۡهِمۡ طَيِّبَٰتٍ أُحِلَّتۡ لَهُمۡ وَبِصَدِّهِمۡ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ كَثِيرٗا
Basi kwa sababu ya dhuluma ya Mayahudi, tuliwaharamishia vitu vizuri walivyohalalishiwa. Na kwa sababu ya kuwazuilia kwao watu wengi na Njia ya Mwenyezi Mungu.
Tafsiran larabci:
وَأَخۡذِهِمُ ٱلرِّبَوٰاْ وَقَدۡ نُهُواْ عَنۡهُ وَأَكۡلِهِمۡ أَمۡوَٰلَ ٱلنَّاسِ بِٱلۡبَٰطِلِۚ وَأَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ مِنۡهُمۡ عَذَابًا أَلِيمٗا
Na kuchukua kwao riba, na ilhali walikwishakatazwa hilo, na kula kwao mali ya watu kwa batili. Basi tumewaandalia makafiri katika wao adhabu chungu.
Tafsiran larabci:
لَّٰكِنِ ٱلرَّٰسِخُونَ فِي ٱلۡعِلۡمِ مِنۡهُمۡ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ يُؤۡمِنُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَۚ وَٱلۡمُقِيمِينَ ٱلصَّلَوٰةَۚ وَٱلۡمُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ أُوْلَٰٓئِكَ سَنُؤۡتِيهِمۡ أَجۡرًا عَظِيمًا
Lakini waliobobea katika elimu miongoni mwao, na Waumini, wanayaamini yale yaliyoteremshwa juu yako, na yale yaliyoteremshwa kabla yako. Na wanaosimamisha Sala, na wakatoa Zaka, na wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, hao tutawapa malipo makubwa.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'nisaa
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Wani gungu na cibiyar fassara ta Ruwad ne suka fassarasu tare da haɗin gwiwar Ƙungiyar Da'awa ta Rabwah da Kungiyar hidimtawa abinda Musulunci ya kunsa da yaruka

Rufewa