Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Ayah: (121) Surah: Surah Al-Baqarah
ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَتۡلُونَهُۥ حَقَّ تِلَاوَتِهِۦٓ أُوْلَٰٓئِكَ يُؤۡمِنُونَ بِهِۦۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِهِۦ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ
Wale Mayahudi na Wanaswara tuliowapa Kitabu, wanakisoma kisomo cha sawasawa, wanakifiuata kipasavyo kufuatwa na wanayaamini yaliyomo ndani yake ya kuwaamini Mitume wa Mwenyezi Mungu, ambao miongoni mwao ni wa mwisho wao, Nabii wetu na Mtume wetu Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,. Na hawayapotoi wala hawayabadilishi yaliyokuja ndani yake. Hawa ndio waliomuamini Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na aliyoteremshiwa. Ama wale waliogeuza sehemu ya Kitabu na wakaficha baadhi yake, hao ndio waliomkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na yale aliyoteremshiwa. Na wenye kumkanusha, hao watakuwa ni wetu wenye hasara kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (121) Surah: Surah Al-Baqarah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Terjemahan makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke bahasa Sawahili oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis

Tutup