Check out the new design

Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Fāṭir   Ayah:
وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدۡ كُذِّبَتۡ رُسُلٞ مِّن قَبۡلِكَۚ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ
Na watu wako wakikukanusha, ewe Mtume, kwa hakika wamekanushwa Mitume kabla yako wewe. Na kwa Mwenyezi Mungu mambo yanaishia huko Akhera, basi hapo Atamlipa kila mmoja anachostahili. Katika hii pana kumliwaza Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tafsir berbahasa Arab:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٞۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِٱللَّهِ ٱلۡغَرُورُ
Enyi watu! Hakika agizo la Mwenyezi Mungu la Ufufuzi, malipo mema na mateso ni kweli iliyothibiti, basi yasiwadanganye maisha ya duniani kwa matamanio yake na matakwa yake, wala asiwadanganye Shetani kuhusu Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمۡ عَدُوّٞ فَٱتَّخِذُوهُ عَدُوًّاۚ إِنَّمَا يَدۡعُواْ حِزۡبَهُۥ لِيَكُونُواْ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلسَّعِيرِ
Hakika Shetani ni adui ya binadamu, basi mchukulieni ni adui na msimtii, hakika ni kwamba yeye anawaita wafuasi wake kwenye upotevu ili wawe ni katika watu wa Moto unaowaka.
Tafsir berbahasa Arab:
ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدٞۖ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٞ كَبِيرٌ
Wale waliokataa kwamba Mwenyezi Mungu, Yeye Peke Yake, Ndiye Mola wa kweli, na wakakataa kile walichokuja nacho Mitume Wake, watakuwa na adhabu kali huko Akhera. Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya matendo mema, watapata msamaha kutoka kwa Mola wao na kufutiwa dhambi zao baada ya kuzifanya zisitirike, na watakuwa na malipo mema makubwa, nayo ni Pepo.
Tafsir berbahasa Arab:
أَفَمَن زُيِّنَ لَهُۥ سُوٓءُ عَمَلِهِۦ فَرَءَاهُ حَسَنٗاۖ فَإِنَّ ٱللَّهَ يُضِلُّ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۖ فَلَا تَذۡهَبۡ نَفۡسُكَ عَلَيۡهِمۡ حَسَرَٰتٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِمَا يَصۡنَعُونَ
Je, yule ambaye Shetani anampambia matendo yake maovu ya kumuasi Mwenyezi Mungu, kukufuru na kuwaabudu wasiyekuwa Yeye miongoni mwa waungu na masanamu, akayaona ni mazuri yenye kupendeza, (Je, yeye) ni kama yule ambaye Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Amemuongoza akaliona zuri kuwa ni zuri na ovu kuwa ni ovu? Hakika Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayemtaka na Anamuongoza Anayemtaka. Basi usijiangamize kwa kuwa na huzuni juu ya ukanushaji wa hawa waliopotea. Hakika Mwenyezi Mungu Anayajua maovu yao na Atawalipa kwa hayo malipo mabaya kabisa.
Tafsir berbahasa Arab:
وَٱللَّهُ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ ٱلرِّيَٰحَ فَتُثِيرُ سَحَابٗا فَسُقۡنَٰهُ إِلَىٰ بَلَدٖ مَّيِّتٖ فَأَحۡيَيۡنَا بِهِ ٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ مَوۡتِهَاۚ كَذَٰلِكَ ٱلنُّشُورُ
Na Mwenyezi Mungu Ndiye Ambaye Anapeleka upepo, ukatikisa mawingu, tukayaongoza hadi pale kwenye ardhi kavu, hapo mvua ikateremka, tukahuisha kwa mvua hiyo ardhi baada ya ukavu wake, na hapo mimea ikawa rangi ya kijani. Mfano wa kuhuisha huko, Mwenyezi Mungu Atawahuisha wafu Siku ya Kiyama.
Tafsir berbahasa Arab:
مَن كَانَ يُرِيدُ ٱلۡعِزَّةَ فَلِلَّهِ ٱلۡعِزَّةُ جَمِيعًاۚ إِلَيۡهِ يَصۡعَدُ ٱلۡكَلِمُ ٱلطَّيِّبُ وَٱلۡعَمَلُ ٱلصَّٰلِحُ يَرۡفَعُهُۥۚ وَٱلَّذِينَ يَمۡكُرُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ لَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدٞۖ وَمَكۡرُ أُوْلَٰٓئِكَ هُوَ يَبُورُ
Yoyote yule atakaye enzi ya duniani au Akhera, basi aitake kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na hilo halipatikani isipokuwa kwa kumtii Yeye, kwani enzi yote ni ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kujienzi na kiumbe, Mwenyezi Mungu Atamdhalilisha; na Mwenye kujienzi na Muumba, Mwenyezi Mungu Atamtukuza. Kwake Yeye utajo wake utapanda, na tendo lema Analiinua juu. Na wale wenye kutenda mabaya watapewa adhabu kali. Na vitimbi vya hao vitaangamia na vitaharibika na havitawafaidisha kitu chochote.
Tafsir berbahasa Arab:
وَٱللَّهُ خَلَقَكُم مِّن تُرَابٖ ثُمَّ مِن نُّطۡفَةٖ ثُمَّ جَعَلَكُمۡ أَزۡوَٰجٗاۚ وَمَا تَحۡمِلُ مِنۡ أُنثَىٰ وَلَا تَضَعُ إِلَّا بِعِلۡمِهِۦۚ وَمَا يُعَمَّرُ مِن مُّعَمَّرٖ وَلَا يُنقَصُ مِنۡ عُمُرِهِۦٓ إِلَّا فِي كِتَٰبٍۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٞ
Na Mwenyezi Mungu Alimuumba baba yenu Ādam kwa mchanga kisha Akajaalia kizazi chake kitokamane na maji matwevu, kisha Akawafanya nyinyi ni wanaume na wanawake. Na hakuna mwanamke yoyote anayeshika mimba wala anayezaa isipokuwa Analijua hilo. Na hakuna mtu anayepewa maisha marefu au umri wake ukapunguzwa isipokuwa hayo yamo ndani ya Kitabu kilichoko Kwake, nacho ni Ubao Uliohifadhiwa, kabla mamake hajashika mimba yake na kabla hajamzaa. Hayo yote Mwenyezi Mungu Ameyadhibiti ameyajua kabla hajamuumba, hayataongezwa yale aliyoandikiwa wala hayatapunguzwa. Hakika kule kuwaumba nyinyi, kuzijua hali zenu na kuziandika kwenye Ubao Uliohifadhiwa ni jambo rahisi na sahali kwa Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Fāṭir
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Diterjemahkan oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis.

Tutup