Check out the new design

Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Al-Aḥqāf   Ayah:
۞ وَٱذۡكُرۡ أَخَا عَادٍ إِذۡ أَنذَرَ قَوۡمَهُۥ بِٱلۡأَحۡقَافِ وَقَدۡ خَلَتِ ٱلنُّذُرُ مِنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَمِنۡ خَلۡفِهِۦٓ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّا ٱللَّهَ إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Na kumbuka, ewe Mtume, Nabii wa Mwenyezi Mungu Hūd, ndugu yao kina 'Ād kinasaba na siyo kidini, alipowaonya watu wake kuwa watashukiwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu wakiwa kwenye nyumba zao hapo Aḥqāf (mahali kwenye mchanga mwingi) kusini mwa Arabuni. Na kwa hakika wamepita Mitume wakawaonya watu wao kabla ya Hūd na baada yake wakiwaambia, «Msimshirikishe Mwenyezi Mungu na kitu chochote mnapomuabudu. Mimi nawachelea nyinyi adhabu ya Mwenyezi Mungu katika Siku yenye kituko kikubwa , nayo ni Siku ya Kiyama.»
Tafsir berbahasa Arab:
قَالُوٓاْ أَجِئۡتَنَا لِتَأۡفِكَنَا عَنۡ ءَالِهَتِنَا فَأۡتِنَا بِمَا تَعِدُنَآ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Wakasema, «Je, umetujia kwa ulinganizi wako ili kutuepusha na ibada ya Mola wetu? Basi tuletee hiko unachotuahidi cha adhabu, iwapo wewe ni katika watu wa ukweli wa kauli yako na ahadi yako.»
Tafsir berbahasa Arab:
قَالَ إِنَّمَا ٱلۡعِلۡمُ عِندَ ٱللَّهِ وَأُبَلِّغُكُم مَّآ أُرۡسِلۡتُ بِهِۦ وَلَٰكِنِّيٓ أَرَىٰكُمۡ قَوۡمٗا تَجۡهَلُونَ
Hūd, amani imshukie, akasema, “Hakika ujuzi wa adhabu mliyoahidiwa uko kwa Mwenyezi Mwenyezi Mungu, na kwa kweli mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu, ninawafikishia ujumbe Alionituma nao, na lakini mimi ninawaona kuwa ni watu mlio wajinga kwa kuifanyia haraka adhabu na kuwa na ujasiri juu ya Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
فَلَمَّا رَأَوۡهُ عَارِضٗا مُّسۡتَقۡبِلَ أَوۡدِيَتِهِمۡ قَالُواْ هَٰذَا عَارِضٞ مُّمۡطِرُنَاۚ بَلۡ هُوَ مَا ٱسۡتَعۡجَلۡتُم بِهِۦۖ رِيحٞ فِيهَا عَذَابٌ أَلِيمٞ
Walipoiona adhabu walioifanyia haraka imejitokeza juu ikielekea kwenye mabonde yao, walisema, “Hiki ni kiwingu chenye kutunyesheza mvua.” Hūd, amani imshukie, aliwaambia, «Hiki si kiwingu cha mvua na rehema kama mlivyodhania, bali hiki ni kiwingu cha adhabu mliyoitaka kwa haraka, huo ni upepo ambao ndani yake muna adhabu yenye uchungu na yenye kuumiza.
Tafsir berbahasa Arab:
تُدَمِّرُ كُلَّ شَيۡءِۭ بِأَمۡرِ رَبِّهَا فَأَصۡبَحُواْ لَا يُرَىٰٓ إِلَّا مَسَٰكِنُهُمۡۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
«Unaangamiza kila kitu unachokipitia katika vitu ambavyo ulitumwa uviangamize kwa amri ya Mola wake na matakwa Yake.» Wakawa hakuna kinachoonekana chochote katika miji yao isipokuwa nyumba zao walizokuwa wakizikaa. Mfano wa malipo haya ndiyo tunayowalipa makafiri kwa sababu ya uhalifu wao na kupita kiasi kwao.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَقَدۡ مَكَّنَّٰهُمۡ فِيمَآ إِن مَّكَّنَّٰكُمۡ فِيهِ وَجَعَلۡنَا لَهُمۡ سَمۡعٗا وَأَبۡصَٰرٗا وَأَفۡـِٔدَةٗ فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُمۡ سَمۡعُهُمۡ وَلَآ أَبۡصَٰرُهُمۡ وَلَآ أَفۡـِٔدَتُهُم مِّن شَيۡءٍ إِذۡ كَانُواْ يَجۡحَدُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Na tuliwarahisishia hao 'Ād sababu za kumakinika duniani kwa namna ambayo hatukuwamakinisha nyinyi, enyi Makureshi, na tukawafanya wawe na masikio ya wao kusikia na macho ya wao kuonea na nyoyo za wao kufahamia, wakavitumia katika mambo yanayomfanya Mwenyezi Mungu Awe na hasira nao. Na hilo halikuwafalia kitu chochote kwa kuwa walikuwa wakikanusha hoja za Mwenyezi Mungu, na hiyo adhabu ambayo walikuwa wakiifanyia shere na kuiharakisha. Hili ni onyo kutoka kwa Mwenyezi Mungu, imetukuka shani Yake, na ni tahadharisho kwa wenye kukufuru.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَا مَا حَوۡلَكُم مِّنَ ٱلۡقُرَىٰ وَصَرَّفۡنَا ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ
Hakika tuliiangamiza miji iliyokuwa pambizoni mwenu, enyi watu wa Makkah, kama ile ya kina 'Ād na Thamūd, tukazifanya kuta za nyumba za miji hiyo zimeanguka na kulalia sakafu zake zilizovunjika, na tuliwabainishia watu wa miji hiyo aina za hoja na dalili wapate kurudi nyuma na kuyaacha yale waliokuwa nayo ya ukanushaji Mwenyezi Mungu na aya Zake.
Tafsir berbahasa Arab:
فَلَوۡلَا نَصَرَهُمُ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ قُرۡبَانًا ءَالِهَةَۢۖ بَلۡ ضَلُّواْ عَنۡهُمۡۚ وَذَٰلِكَ إِفۡكُهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Basi si wangaliwasaidia wao, hao tuliowaangamiza miongoni mwa ummah waliopita, waungu wao ambao walichukua kule kuwaabudu ni ibada ya wao kujikurubisha kwa Mola wao, ili wawaombee mbele Yake. Lakini waungu wao waliwapotea, hawakuwaitikia wala hawakuwatetea. Huo ni urongo wao tu na uzushi walioupanga wa kuwafanya wao ni waungu.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Al-Aḥqāf
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Diterjemahkan oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis.

Tutup