Check out the new design

Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Al-Ḥadīd   Ayah:
لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَأَنزَلۡنَا مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمِيزَانَ لِيَقُومَ ٱلنَّاسُ بِٱلۡقِسۡطِۖ وَأَنزَلۡنَا ٱلۡحَدِيدَ فِيهِ بَأۡسٞ شَدِيدٞ وَمَنَٰفِعُ لِلنَّاسِ وَلِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ مَن يَنصُرُهُۥ وَرُسُلَهُۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ إِنَّ ٱللَّهَ قَوِيٌّ عَزِيزٞ
Hakika tumetumiliza Mitume wetu kwa hoja zilizo wazi na kuwateremshia Vitabu vyenye hukumu na sheria, na tukateremsha mizani ili watu waamiliane baina yao kwa uadilifu, na tukateremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa mengi kwa watu, na ili Mwenyezi Mungu Amjue, ujuzi wenye kujitokeza kwa watu, yule anayetetea Dini Yake na Mitume Wake kwa ghaibu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Asiyetendeshwa nguvu, ni Mshindi hakuna anayeweza kushindana na Yeye.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحٗا وَإِبۡرَٰهِيمَ وَجَعَلۡنَا فِي ذُرِّيَّتِهِمَا ٱلنُّبُوَّةَ وَٱلۡكِتَٰبَۖ فَمِنۡهُم مُّهۡتَدٖۖ وَكَثِيرٞ مِّنۡهُمۡ فَٰسِقُونَ
Na hakika tuliwatumiliza Nūḥ na Ibrāhīm kwa watu wao, na tukajaalia kwenye kizazi chao unabii na vitabu vilivyoteremshwa. Basi miongoni mwa watu wa kizazi chao kuna walioongoka kwenye haki, na wengi kati yao wametoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ قَفَّيۡنَا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم بِرُسُلِنَا وَقَفَّيۡنَا بِعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَ وَءَاتَيۡنَٰهُ ٱلۡإِنجِيلَۖ وَجَعَلۡنَا فِي قُلُوبِ ٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُ رَأۡفَةٗ وَرَحۡمَةٗۚ وَرَهۡبَانِيَّةً ٱبۡتَدَعُوهَا مَا كَتَبۡنَٰهَا عَلَيۡهِمۡ إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ رِضۡوَٰنِ ٱللَّهِ فَمَا رَعَوۡهَا حَقَّ رِعَايَتِهَاۖ فَـَٔاتَيۡنَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنۡهُمۡ أَجۡرَهُمۡۖ وَكَثِيرٞ مِّنۡهُمۡ فَٰسِقُونَ
Kisha tukafuatisha, kwenye athari za Nūḥ na Ibrāhīm, Mitume wetu tiliowatumiliza kwa hoja zilizo wazi, na tukamfuatisha 'Īsā mwana wa Maryam na tukampa Injili, na tukajaalia ndani ya nyoyo za wale waliomfuata na kuwa kwenye dini yake ulaini na huruma, wakawa wanapendana wao kwa wao, na walizusha taratibu za kuabudu, kwa kupitisha kiasi katika ibada, ambazo hatukuwalazimisha nazo isipokuwa ni wao wenyewe waliojilazimisha nazo kwa lengo la kupata radhi za Mwenyezi Mungu, lakini hawakusimama nazo vile inavyotakiwa kusimama. Basi tukawapa wale walioamini miongoni mwao malipo yao kulingana na Imani yao, na wengi miongoni mwao ni wenye kutoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu na ni wenye kumkanusha Nabii Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tafsir berbahasa Arab:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَءَامِنُواْ بِرَسُولِهِۦ يُؤۡتِكُمۡ كِفۡلَيۡنِ مِن رَّحۡمَتِهِۦ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ نُورٗا تَمۡشُونَ بِهِۦ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Enyi mlioamini! Fuateni amri za Mwenyezi Mungu na mjiepushe na makatazo Yake na muaminini Mtume Wake, Atawapa rehema Zake mara mbili zaidi, na Atawafanya muwe na nuru ambayo kwayo mnajiongoza na Atawasamehe dhambi zenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa waja Wake, ni Mwenye kuwarehemu.
Tafsir berbahasa Arab:
لِّئَلَّا يَعۡلَمَ أَهۡلُ ٱلۡكِتَٰبِ أَلَّا يَقۡدِرُونَ عَلَىٰ شَيۡءٖ مِّن فَضۡلِ ٱللَّهِ وَأَنَّ ٱلۡفَضۡلَ بِيَدِ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Amewapa haya yote ili wapate kujua watu waliopewa Vitabu ambao hawakumuamini Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwamba wao hawawezi chochote kujipa wao wenyewe nyongeza za kheri za Mwenyezi Mungu wala kuwapatia wengine, na kwamba nyongeza zote ziko kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wema mkubwa na vipewa vingi kwa viumbe Vyake.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Al-Ḥadīd
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Diterjemahkan oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis.

Tutup