Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Ayah: (22) Surah: Surah Al-Mujādilah
لَّا تَجِدُ قَوۡمٗا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ يُوَآدُّونَ مَنۡ حَآدَّ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَوۡ كَانُوٓاْ ءَابَآءَهُمۡ أَوۡ أَبۡنَآءَهُمۡ أَوۡ إِخۡوَٰنَهُمۡ أَوۡ عَشِيرَتَهُمۡۚ أُوْلَٰٓئِكَ كَتَبَ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلۡإِيمَٰنَ وَأَيَّدَهُم بِرُوحٖ مِّنۡهُۖ وَيُدۡخِلُهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ رَضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ أُوْلَٰٓئِكَ حِزۡبُ ٱللَّهِۚ أَلَآ إِنَّ حِزۡبَ ٱللَّهِ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Hutakuta, ewe Mtume, watu wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na wanaofanya matendo waliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu, wakiwapenda na kuwategemea wale wanaomsimamishia uadui Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wanaoenda kinyume na amri zao, ingawa ni baba zao au wana wao au ndugu zo au jamaa zao wa karibu. Hao wanaofunga urafiki kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wanaosimamisha uadui kwa ajili Yake ndio wale ambao Mwenyezi Mungu Ameithibitisha Imani ndani ya nyoyo zao na Akawatia nguvu kwa kuwapa ushindi utokao Kwake na msaada dhidi ya adui yao duniani, na Atawaingiza huko Akhera kwenye mabustani ya Peponi ambayo chini ya miti yake inapita mito, hali ya kukaa humo muda mrefu usiomalizika, Amewapa radhi Zake na hatawakasirikia na wao wameridhika na Mola wao kwa yale Aliyowapatia ya utukufu na daraja kubwa. Hao ndio kundi la Mwenyezi Mungu na walioshikana na Yeye, na hao ndio wenye kufaulu kwa kupata furaha ya duniani na Akhera.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (22) Surah: Surah Al-Mujādilah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Terjemahan makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke bahasa Sawahili oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis

Tutup