Check out the new design

Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Al-Ḥāqqah   Ayah:
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ
wala hatakuwa na chakula isipokuwa kile kinachotokana na usaa wa watu wa motoni,
Tafsir berbahasa Arab:
لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ
hakuna mwenye kukila isipokuwa wale wenye dhambi, wanaoshikilia kumkanusha Mwenyezi mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ
Naapa kwa mnavyoviona miongoni mwa vitu vinavyooonekana,
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ
na vile msivyoviona miongoni mwa vile vilivyoghibu kwenu., hakika Qur’ani ni maneno ya Mwenyezi Mungu.
Tafsir berbahasa Arab:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Inasomwa na mjumbe mkubwa wa cheo na utukufu.
Tafsir berbahasa Arab:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ
Na si maneno ya mshairi kama mnavyodai, ni uchache mno mnavyoamini.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala si tungo kama zile tungo za makuhani, ni kuchache mno kule kukumbuka kwenu na kutia akilini kuwa kuna tafauti baina ya mawili hayo.
Tafsir berbahasa Arab:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Lakini hiyo Qur’ani ni maneno ya Mola wa viumbe wote Aliyoyateremshia Mtume Wake Muhaammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ
Na lau Muhammad angalitusingizia maneno tusiyoyanena
Tafsir berbahasa Arab:
لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ
tungalimtesa na tungalimkamata kwa nguvu na uweza, kwani nguvu ya kila kitu iko kwenye upande wake wa kulia,
Tafsir berbahasa Arab:
ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ
kisha tungalimkata mshipa wa moyo wake.,
Tafsir berbahasa Arab:
فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ
hataweza yoyote kuyazuia mateso yetu yasimpate.
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ
Na hii Qur’ani ni mawaidha kwa wachamungu wanaofuata amri za Mwenyezi Mungu na kuyaepuka makatazo yake.
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Na sisi kwa hakika tunajua kwamba miongoni mwenu kuna wanaoikanusha hii Qur’ani pamoja na kuwa dalili zake ziko wazi.
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na kwa hakika kuikanusha Qur’ani ni majuto makubwa kwa wenye kuikanusha pindi watakapoiona adhabu yao na kuona starehe za wenye kuiamini.
Tafsir berbahasa Arab:
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Na kwa hakika hii Qur’ani ni haki iliyothibiti na yakini isiyo na shaka.
Tafsir berbahasa Arab:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi Mwepushie Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kila sifa isiyonasibiana na haiba Yake, na umtaje kwa jina Lake tukufu.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Al-Ḥāqqah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Diterjemahkan oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis.

Tutup