Na badala ya Mwenyezi Mungu wanawaabudu wasio wamilikia riziki kutoka mbinguni wala kwenye ardhi, wala hawawezi kitu.
Na wakawa badala ya Mwenyezi Mungu wakaabudu masanamu ambayo hayawezi kuwapa riziki yoyote hata chembe, sawa sawa ikiwa riziki hiyo inatoka mbinguni kama maji, au kutokana na ardhi kama matunda ya miti na mimea. Na miungu hiyo haiwezi kufanya lolote kama hayo, wala duni ya hayo!
Basi msimpigie Mwenyezi Mungu mifano. Hakika Mwenyezi Mungu anajua,na nyinyi hamjui.
Na ilivyo kuthibitikieni kuwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu hakufaeni kitu, basi msiseme kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ana yeyote wa kumshabihi, ikawa kisingizio cha kuwaabudu hao kwa vipimo vipotovu, na kushabihisha kusio kweli kwa ajili ya kuwaabudu hao pamoja naye! Hakika Mwenyezi Mungu anajua upotovu wa mnayo yatenda, naye atakulipeni kwayo na hali nyinyi mmo katika mghafala hamjui ubaya wa mwisho wenu!
Mwenyezi Mungu anapiga mfano wa mtumwa aliye milikiwa, asiyeweza kitu, na mwingine tuliye mruzuku riziki njema inayo toka kwetu,naye akawa anatoa katika riziki hiyo kwa siri na dhaahiri. Je, hao watakuwa sawa? Alhamdu Lillahi! Kuhimidiwa kote ni kwa Mwenyezi Mungu.Lakini wengi wao hawajui.
* Mwenyezi Mungu amepiga mfano kufahamisha ufisadi walio nao washirikina. Mtumwa aliye milikiwa kama mtumwa mamluki, hanalo aliwezalo kulitenda; na muungwana anaye ruzukiwa na Mwenyezi Mungu riziki ya halali, naye anatoa katika hiyo riziki kwa siri na dhaahiri! Je, ni sawa watumwa wasio weza kitu, na waungwana wenye nacho na wanatumia walicho nacho? Hakika Mwenyezi Mungu anamiliki kila kitu, na anafanya katika ufalme wake kama apendavyo. Na asiye kuwa Yeye hamiliki chochote. Basi huyo hastahiki kuabudiwa na kuhimidiwa. Sifa zote ni haki ya Mwenyezi Mungu peke yake. Yeye ndiye Mwenye Utukufu peke yake, kwani kila kheri inatoka kwake, na kila zuri linarejea kwake. Wala hawatendi hao wanayo yatenda kwa kujua, bali wanatenda kwa kuwafuata wakubwa zao. Bali wengi wao hawajui, na wanaziambatisha neema za Mwenyezi Mungu kwa wengineo, na wanawaabudu hao badala yake!
Na Mwenyezi Mungu anapiga mfano wa watu wawili. Mmoja wao ni bubu, hawezi chochote, naye ni mzigo kwa bwana wake. Popote anapo muelekeza haleti kheri. Je! Huyo anaweza kuwa sawa na yule anaye amrisha uadilifu,naye yuko juu ya Njia Iliyo Nyooka.
Mwenyezi Mungu amekupigieni mfano mwengine, wa watu wawili. Mmoja wao kiziwi-bubu; hafahamu wala hafahamiki, mzigo kwa aliye mlazimu kumtazama. Bwana wake akimuelekeza kokote harejei na faida yoyote. Basi, je, mtu huyu atakuwa sawa na mtu mwenginewe aliye fasihi wa kusema, anasikia vyema, anaamrisha haki na uadilifu, naye mwenyewe ameshika Njia iliyo kaa sawa, isiyo kwenda upogo? Huyo kiziwi asiye sikia wala kusema wala hafahamu wala hafahamiki, ndio mfano wa masanamu wanayo yaabudu badala ya Mwenyezi Mungu. Kwani hayo hayasikii wala hayasemi wala hayafai kitu. Hayawezi hayo kulingana na Mwenye kusikia, Mwenye kujua, Mwenye kuwaita watu wende kwenye kheri na haki, na kwenye Njia Iliyo Nyooka.
Na siri zote za katika mbingu na ardhi ziko kwa Mwenyezi Mungu.Wala halikuwa jambo la Saa (ya Kiyama) ila kama kupepesa kwa jicho, au akali ya hivyo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
Na ni ya Mwenyezi Mungu tu peke yake yote wasiyo yajua waja katika mbingu na katika ardhi. Wala jambo la kuja Siku ya Kiyama, na kufufuliwa watu, haraka yake na upesi wake kwa Mwenyezi Mungu, si chochote ila ni kama kufumba na kufumbua jicho! Bali ni duni kuliko hivyo, jinsi ya upesi wake. Hakika uwezo wa Mwenyezi Mungu ni mkubwa mno, Yeye haemewi na kitu.
Na Mwenyezi Mungu amekutoeni matumboni mwa mama zenu, hali ya kuwa hamjui kitu, na amekujaalieni masikio na macho na nyoyo ili mpate kushukuru.
Na Mwenyezi Mungu amekutoeni kutokana na matumbo ya mama zenu hali hamjui chochote katika yaliyo kuzungukeni. Na akakupeni kusikia na kuona na nyoyo, kuwa ndio silaha za kujifunzia na kufahamu, ili mpate kumuamini kwa njia ya ilimu, na mumshukuru kwa alivyo kufadhilini. Utabibu wa kisasa umethibitisha kuwa kuweza kusikia kunaanza mapema sana katika maisha ya mtoto mchanga, mnamo wiki chache za mwanzo. Ama kuona huanza mwezi wa tatu. Wala kuona hakuwi baraabara mpaka katika mwezi wa sita. Ama "moyo " wa kufahamu na kutambua huwa baada ya hayo. Mpango ulio letwa na Qur'ani ni mpango unao lingana na hisiya hizo.
Je! Hawawaoni ndege walivyo wat'iifu katika anga la mbingu? Hapana mwenye kuwashika isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Hakika katika haya zipo ishara kwa watu wanao amini.
Je! Hao washirikina hawawaangalii ndege walio jaaliwa waweze kuruka hewani juu, kwa kupewa na Mwenyezi Mungu mbawa kubwa kuliko miili yao, wakiikunjua na kuikunja. Na Mwenyezi Mungu akaidhalilisha hewa kuwabeba hao ndege. Hapana anaye washika huko angani ila Mwenyezi Mungu kwa nidhamu aliyo itengeneza Yeye Mwenyewe! Hakika katika kuwatazama hao ndege, na kuzingatia hikima ya Mwenyezi Mungu katika kuwaumba, ni ishara kubwa ya kuwanafiisha walio kuwa tayari kuamini. Ndege wanaruka kwa sababu kadhaa wa kadhaa katika kuumbwa kwao. Muhimu kuliko yote ni lile umbo lao la kuchongoka, na kuwa mbawa zao zilivyo tanda zenye manyoya, na mafupa yenye uwazi na myepesi na vifuko vya hewa kati ya matumbo yao, navyo vimeambatishwa na mayavuyavu (mapafu). Hivyo vifuko hujaa hewa wakati wa kuruka, basi huzidi hao ndege kuwa wepesi.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
Hasil pencarian:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".