Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani * - Daftar isi terjemahan

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Terjemahan makna Ayah: (71) Surah: Surah An-Naḥl
وَٱللَّهُ فَضَّلَ بَعۡضَكُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ فِي ٱلرِّزۡقِۚ فَمَا ٱلَّذِينَ فُضِّلُواْ بِرَآدِّي رِزۡقِهِمۡ عَلَىٰ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَهُمۡ فِيهِ سَوَآءٌۚ أَفَبِنِعۡمَةِ ٱللَّهِ يَجۡحَدُونَ
Na Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine katika riziki. Na wale walio fadhilishwa hawarudishi riziki zao kwa wale ilio wamiliki mikono yao ya kulia ili wawe sawa katika riziki hiyo. Basi je, wanazikataa neema za Mwenyezi Mungu?
Na Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kwa riziki kuliko wengineo. Amemruzuku bwana mwenye kumiliki kuliko mtumwa mamluki. Wala walio ruzukiwa kingi hawawapi watumwa wao hata nusu ya riziki yao, ili wapate kuwa wote na riziki sawa! Basi ikiwa hawa makafiri hawakubali watumwa wao washirikiane nao katika riziki iliyo toka kwa Mwenyezi Mungu, nao wote ni wanaadamu kama wao, basi vipi wao wanataka kumshirikisha Mwenyezi Mungu na viumbe vyake katika mambo yasio kuwa laiki naye Subhanahu wa Taa'la, nako ni kustahiki kuabudiwa? Basi je, macho ya hao washirikina yataendelea kufumbika baada ya yote haya, wakabaki wakipinga neema za Mwenyezi Mungu juu yao kwa kumshirikisha Yeye na wengineo?
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (71) Surah: Surah An-Naḥl
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani - Daftar isi terjemahan

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

Tutup