Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani * - Daftar isi terjemahan

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Terjemahan makna Ayah: (266) Surah: Surah Al-Baqarah
أَيَوَدُّ أَحَدُكُمۡ أَن تَكُونَ لَهُۥ جَنَّةٞ مِّن نَّخِيلٖ وَأَعۡنَابٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ لَهُۥ فِيهَا مِن كُلِّ ٱلثَّمَرَٰتِ وَأَصَابَهُ ٱلۡكِبَرُ وَلَهُۥ ذُرِّيَّةٞ ضُعَفَآءُ فَأَصَابَهَآ إِعۡصَارٞ فِيهِ نَارٞ فَٱحۡتَرَقَتۡۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَتَفَكَّرُونَ
Je! Yupo mmoja wenu anaye penda kuwa na kitalu cha mitende na mizabibu ipitayo mito kati yake, naye humo hupata mazao ya kila namna, na uzee ukamfikia naye hali ana watoto wanyonge, kikapigwa na kimbunga chenye moto, kikaungua? Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu anavyo kubainishieni Ishara ili mpate kufikiri.
Hapana yeyote katika nyinyi anaye penda kuwa na kitalu cha mitende na mizabibu na mito inapita kati yake na kimezaa kila namna ya matunda ayatakayo, naye hali amekwisha kuwa mkongwe na akawa na watoto wadogo wanyonge hawawezi kazi wala yeye hajiwezi kwa ukongwe wake, kikaja kitalu chake kikakauka kwa upepo mkali wenye moto, na miti ikaungua, wakati ambao yeye mwenyewe na watoto ndio wamo katika shida ya kuhitaji. Basi hali kadhaalika shani ya mwenye kutoa sadaka na akafuatishia masimbulizi na maudhi na riya, kujionyesha kwa watu, ambayo hayo yakapoteza thawabu zote za sadaka zake, na wala hawezi tena kutoa sadaka kwa kujitengezea nafsi yake. Kwa bayana kama hizi ndio Mwenyezi Mungu anakuonyesheni Ishara ili mpate kutafakari na kujifunza. Ilimu ya kisasa inaeleza kuwa katika anga pepo kali hugongana zikatoka radi na umeme na mvua. Huenda ukatokea moto kwa umeme kwa kugongana mawingu, au pengine huweza kutokea vimondo kutokana na volkano (burkani) iliyo karibu ikateketeza miti na chochote kilicho katika sehemu hizo. Qur'ani inaashiria maana zote hizo.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (266) Surah: Surah Al-Baqarah
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani - Daftar isi terjemahan

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

Tutup