Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani * - Daftar isi terjemahan

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Terjemahan makna Ayah: (59) Surah: Surah An-Nisā`
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَأُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنكُمۡۖ فَإِن تَنَٰزَعۡتُمۡ فِي شَيۡءٖ فَرُدُّوهُ إِلَى ٱللَّهِ وَٱلرَّسُولِ إِن كُنتُمۡ تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ ذَٰلِكَ خَيۡرٞ وَأَحۡسَنُ تَأۡوِيلًا
Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema.
Enyi mlio sadiki aliyo kuja nayo Muhammad! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume, na wale wanao tawala mambo yenu miongoni mwa Waislamu wanao simama juu ya haki na uadilifu, na wanatekeleza Sharia ya Mwenyezi Mungu. Na mkizozana katika jambo baina yenu basi rejeeni kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake ili mpate kujua hukumu yake. Kwani Yeye Mwenyezi Mungu amekuteremshieni Kitabu chake na Mtume wake amebainisha hicho Kitabu. Na katika hayo ipo hukumu ya hayo mnayo khitalifiana kwayo. Haya ni kwa mujibu wa Imani yenu kumuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na haya ndio bora kwenu ili mpate kuongoka kwendea uadilifu katika mnayo khitalifiana kwayo, na mwisho wake ndio mzuri zaidi. Kwani hivyo ndio kuzuia zisitokee khilafu zinazo pelekea ugomvi na upotovu.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (59) Surah: Surah An-Nisā`
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani - Daftar isi terjemahan

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

Tutup