Check out the new design

Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Sura: Al-‘Ankabût   Versetto:

Al-Ankabut

الٓمٓ
«Alif, Lām, Mīm.» Yametangulia maelezo juu ya herufi zilizokatwa na kutengwa mwanzo wa sura ya Al-Baqarah.
Esegesi in lingua araba:
أَحَسِبَ ٱلنَّاسُ أَن يُتۡرَكُوٓاْ أَن يَقُولُوٓاْ ءَامَنَّا وَهُمۡ لَا يُفۡتَنُونَ
Je wanadhani watu kwamba wakisema «Tumeamini» Mwenyezi Mungu Atawaachilia bila ya kuwajaribu wala kuwatahini?
Esegesi in lingua araba:
وَلَقَدۡ فَتَنَّا ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۖ فَلَيَعۡلَمَنَّ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ صَدَقُواْ وَلَيَعۡلَمَنَّ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Kwa hakika, tuliwajaribu wale waliokuwa kabla yao miongoni mwa ummah mbalimbali na tukawatahini kwa Mitume wetu tuliowatumiliza kwao. Basi hakika ni kwamba Mwenyezi Mungu Atawajua, ujuzi wa kujitokeza nje kwa viumbe, ukweli wa wale wakweli katika Imani yao na urongo wa warongo, ili Alipambanue kila kundi na lingine.
Esegesi in lingua araba:
أَمۡ حَسِبَ ٱلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ أَن يَسۡبِقُونَاۚ سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ
Je, kwani wanadhani wale wanaofanya mambo ya uasi, ya ushirikina na mengineyo, kuwa watatushinda wajikwepeshe na sisi tusiwaweze? Ni uamuzi mbaya mno wanaouamua.
Esegesi in lingua araba:
مَن كَانَ يَرۡجُواْ لِقَآءَ ٱللَّهِ فَإِنَّ أَجَلَ ٱللَّهِ لَأٓتٖۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Yoyote mwenye kuwa na matumaini ya kukutana na Mwenyezi Mungu na akawa na matarajio ya kupata malipo Yake mema, basi muda Aliouweka Mwenyezi Mungu wa kuwafufua viumbe Wake ili wahesabiwe na walipwe ni wenye kuja hivi karibuni. Na Yeye Ndiye Msikizi wa maneno, Mjuzi wa vitendo.
Esegesi in lingua araba:
وَمَن جَٰهَدَ فَإِنَّمَا يُجَٰهِدُ لِنَفۡسِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَغَنِيٌّ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na mwenye kupigana jihadi katika njia ya kuinua neno la Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na akapigana jihadi na nafsi yake kwa kuisukuma ifanye vitendo vya utiifu, basi anapigana jihadi kwa maslahi ya nafsi yake. Kwa kuwa yeye anafanya hilo kwa kutaka thawabu ya kupigana kwake jihadi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Hana haja ya matendo mema ya waja Wake, kwani mamlaka ni Yake, uumba na mapitisho.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Al-‘Ankabût
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione di Abdullah Mohammed Abu Bakr e Shaikh Nasser Khamis.

Chiudi