Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Versetto: (153) Sura: Al ‘Imrân
۞ إِذۡ تُصۡعِدُونَ وَلَا تَلۡوُۥنَ عَلَىٰٓ أَحَدٖ وَٱلرَّسُولُ يَدۡعُوكُمۡ فِيٓ أُخۡرَىٰكُمۡ فَأَثَٰبَكُمۡ غَمَّۢا بِغَمّٖ لِّكَيۡلَا تَحۡزَنُواْ عَلَىٰ مَا فَاتَكُمۡ وَلَا مَآ أَصَٰبَكُمۡۗ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Kumbukeni, enyi maswahaba wa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hali zenu zilivyokuwa, mlipokuwa mnalipanda jabali mkiwakimbia maadui zenu, wala hamgeuki kumwangalia yoyote kwa sababu ya yale yaliyowafikia ya babaiko, kuogopa na fazaa. Na huku Mtume wa Mwenyezi Mungu , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, amekita kwenye uwanja wa vita, anawaita nyuma yenu kwa kuwaambia, «Njooni kwangu, enyi waja wa Mwenyezi Mungu,» hali ya kuwa nyinyi hamsikii wala hamuangalii. Hapo yakawa malipo yenu ni kupatwa na machungu, dhiki na kero. Aliyafanya hayo Mwenyezi Mungu ili msihuzunike kwa mliyoyakosa ya ushindi na ngawira wala yaliyowafikia ya kuingiwa na kicho na kushindwa. Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa matendo yenu yote; hakuna chochote katika hayo kinachofichika Kwake.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (153) Sura: Al ‘Imrân
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi