Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Versetto: (81) Sura: Al ‘Imrân
وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ لَمَآ ءَاتَيۡتُكُم مِّن كِتَٰبٖ وَحِكۡمَةٖ ثُمَّ جَآءَكُمۡ رَسُولٞ مُّصَدِّقٞ لِّمَا مَعَكُمۡ لَتُؤۡمِنُنَّ بِهِۦ وَلَتَنصُرُنَّهُۥۚ قَالَ ءَأَقۡرَرۡتُمۡ وَأَخَذۡتُمۡ عَلَىٰ ذَٰلِكُمۡ إِصۡرِيۖ قَالُوٓاْ أَقۡرَرۡنَاۚ قَالَ فَٱشۡهَدُواْ وَأَنَا۠ مَعَكُم مِّنَ ٱلشَّٰهِدِينَ
kumbuka, ewe Mtume, pindi Alipochukua Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, ahadi ya mkazo kwa Manabii wote kwamba, «Nikiwaletea Kitabu na hekima kisha akaja kwenu mjumbe kutoka kwangu, mwenye kusadikisha vitabu mlivyonavyo, mtamuamini na kumnusuru? Je, mumekiri na kukubali hilo na mumechukua juu yake ahadi yangu ya mkazo?» Wakasema, «Tumekubali hilo.» Akasema, «Kueni mashahidi, baadhi yenu juu ya wengine, na kueni mashahidi kwa hilo juu ya ummah wenu, na mimi ni Mwenye kushuhudia pamoja na nyinyi juu yenu na juu yao. Katika haya pana ahadi nzito Aliyoichukua Mwenyezi Mungu kutoka kwa kila Nabii amuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kuchukua ahadi nzito kutoka kwa ummah wa Manabii wote juu ya hilo.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (81) Sura: Al ‘Imrân
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi