Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Versetto: (25) Sura: Al-Fath
هُمُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَصَدُّوكُمۡ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَٱلۡهَدۡيَ مَعۡكُوفًا أَن يَبۡلُغَ مَحِلَّهُۥۚ وَلَوۡلَا رِجَالٞ مُّؤۡمِنُونَ وَنِسَآءٞ مُّؤۡمِنَٰتٞ لَّمۡ تَعۡلَمُوهُمۡ أَن تَطَـُٔوهُمۡ فَتُصِيبَكُم مِّنۡهُم مَّعَرَّةُۢ بِغَيۡرِ عِلۡمٖۖ لِّيُدۡخِلَ ٱللَّهُ فِي رَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۚ لَوۡ تَزَيَّلُواْ لَعَذَّبۡنَا ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ عَذَابًا أَلِيمًا
Makafiri wa Kikureshi ndio waliokataa kumpwekesha Mwenyezi Mungu, wakawazuia nyinyi, Siku ya Ḥudaybiyah, kuingia Msikiti wa al-Ḥarām, wakakataza wanyama na wakawafunga wasifike mahali pa wao kuchinjwa, napo ni Ḥarām. Na lau si wanaume Waumini walio wanyonge na wanawake Waumini msiowajua, walio kati ya hawa makafiri wa Makkah, wanaoificha Imani yao kwa kuzichelea nafsi zao, msije mkawakanyaga kwa jeshi lenu mkawaua, mkapata dhambi, aibu na gharama kwa mauaji hayo bila kujua, tungaliwapa nyinyi uwezo juu yao, ili Mwenyezi Mungu Apate kumtia kwenye rehema Zake Anayemtaka kwa kumpa neema ya kuamini baada ya kukanusha. Lau hawa Waumini wa kiume na Waumini wa kike wangalitenganika na washirikina wa Makkah na wakajitoa kati yao, tungaliwaadhibu wale waliokufuru na kukanusha miongoni mwao adhabu yenye uchungu na kuumiza.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (25) Sura: Al-Fath
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi