Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Versetto: (12) Sura: Al-An‘âm
قُل لِّمَن مَّا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ قُل لِّلَّهِۚ كَتَبَ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۚ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Ni ya nani mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake?» Sema, «Ni ya Mwenyezi Mungu. Na kama mnavyolikubali hilo na kulijua, basi muabuduni Yeye Peke Yake. Mwenyezi Mungu Amechukua ahadi juu ya nafsi Yake kurehemu, Hatawaangusiliza waja Wake kwa kuwatesa. Kwa hakika Atawakusanya nyinyi kwenye Siku ya Kiyama ambayo haina shaka ili mhesabiwe na mlipwe. Wale waliomshirikisha Mwenyezi Mungu wamejiangamiza nafsi zao; wao hawampwekeshi Mwenyezi Mungu wala hawaiamini ahadi Yake ya Pepo na Moto na hawaukubali unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (12) Sura: Al-An‘âm
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi