Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Versetto: (12) Sura: Yûnus
وَإِذَا مَسَّ ٱلۡإِنسَٰنَ ٱلضُّرُّ دَعَانَا لِجَنۢبِهِۦٓ أَوۡ قَاعِدًا أَوۡ قَآئِمٗا فَلَمَّا كَشَفۡنَا عَنۡهُ ضُرَّهُۥ مَرَّ كَأَن لَّمۡ يَدۡعُنَآ إِلَىٰ ضُرّٖ مَّسَّهُۥۚ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلۡمُسۡرِفِينَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Na mtu akiguswa na shida hutuomba naye kaegesha ubavu, au kakaa, au kasimama. Lakini tukimwondoshea shida yake huendelea kama kwamba hakupata kutuomba tumwondoshee shida iliyo mpata. Ndio namna hiyo wamepambiwa warukao mipaka yale waliyo kuwa wakiyatenda.
Na mtu akisibiwa na madhara katika nafsi yake au mali yake au mfano wa hayo, huhisi unyonge wake, na humwomba Mola wake Mlezi kwa hali yoyote - akiwa kajinyoosha, au kakaa kitako, au kasimama - amwondolee dhiki zake! Mwenyezi Mungu akisha mwitikia, na akamwondolea hizo shida zake, humuacha kando Mwenyezi Mungu na akaendelea na maasi yake, na akasahau fadhila za Mwenyezi Mungu juu yake, kama kwamba hakupatikana na madhara yoyote, wala hajapata kumwomba amwondolee! Na mfano wa mtindo huu Shetani ndio huwazaini Makafiri, akawapambia vitendo vyao viovu, na uzushi wao mpotovu, wakaona yote hayo ni mazuri.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (12) Sura: Yûnus
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi