Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Versetto: (15) Sura: Yûnus
وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَاتُنَا بَيِّنَٰتٖ قَالَ ٱلَّذِينَ لَا يَرۡجُونَ لِقَآءَنَا ٱئۡتِ بِقُرۡءَانٍ غَيۡرِ هَٰذَآ أَوۡ بَدِّلۡهُۚ قُلۡ مَا يَكُونُ لِيٓ أَنۡ أُبَدِّلَهُۥ مِن تِلۡقَآيِٕ نَفۡسِيٓۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّۖ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Na wanapo somewa Aya zetu zilizo wazi, wale wasio taraji kukutana na Sisi husema: Lete Qur'ani isiyo kuwa hii, au ibadilishe. Sema: Hainifalii mimi kuibadilisha kwa nitakavyo nafsi yangu. Mimi sifuati ila ninayo funuliwa kwa Wahyi. Hakika mimi naogopa, nikimuasi Mola wangu Mlezi, adhabu ya Siku iliyo kuu.
Zilipo dhihiri Aya (Ishara) za Qur'ani kutokana na Mtume wetu Muhammad juu ya washirikina, walisema makafiri wasio ikhofu adhabu ya Mwenyezi Mungu wala hawataraji thawabu zake: Tuletee kitabu kinginecho kisicho kuwa hii Qur'ani. Au badilisha yaliyomo humu, yale yasiyo tupendeza. Waambie ewe Mtume: Hayumkini wala haijuzu mimi kugeuza au kubadilisha kwa nafsi yangu. Mimi si chochote ila ni mwenye kufuata na mwenye kufikisha kile kinacho funuliwa kwangu kutokana na Mola wangu Mlezi. Mimi naogopa, nikienda kinyume na Wahyi, Ufunuo, wa Mola wangu Mlezi, adhabu ya Siku ambayo khatari yake ni kuu, na kitisho chake ni kikubwa!
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (15) Sura: Yûnus
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi