Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Versetto: (39) Sura: Yûnus
بَلۡ كَذَّبُواْ بِمَا لَمۡ يُحِيطُواْ بِعِلۡمِهِۦ وَلَمَّا يَأۡتِهِمۡ تَأۡوِيلُهُۥۚ كَذَٰلِكَ كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلظَّٰلِمِينَ
Bali wameyakanusha wasio yaelewa ilimu yake kabla hayajawajia maelezo yake. Kadhaalika walio kabla yao walikanusha vile vile. Basi angalia jinsi ulivyo kuwa mwisho wa madhaalimu hao.
Bali hawa washirikina wamekimbilia kuikadhibisha Qur'ani bila ya kuzingatia, wakajua yaliomo ndani yake! Wao wenyewe hawakutazama mna nini, wala hawakusita kuitafuta tafsiri yake, na kutaka kuelewa hukumu zake kwa kuwauliza wenginewe! Na kukadhibisha namna hii bila ya ujuzi, ndivyo walivyo wakanusha makafiri wa kaumu za zamani Mitume wao na Vitabu vyao! Basi, ewe mwanaadamu! Angalia yaliishiaje mambo ya walio kadhibisha walio tangulia. Waliachiliwa mbali na wakateketezwa kwa adhabu! Na huu ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu kwa mfano wa hao.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (39) Sura: Yûnus
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi