Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Versetto: (90) Sura: An-Nahl
۞ إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُ بِٱلۡعَدۡلِ وَٱلۡإِحۡسَٰنِ وَإِيتَآيِٕ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَيَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِ وَٱلۡبَغۡيِۚ يَعِظُكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha kufanya uadilifu, na hisani,na kuwapa jamaa; na anakataza uchafu, na uovu, na dhulma. Anakuwaidhini ili mpate kukumbuka.
Mwenyezi Mungu anawaamrisha waja wake uadilifu wa maneno na vitendo, na katika kila jambo wakusudie lilio bora, na walifadhilishe kuliko jenginelo. Kama anavyo amrisha kuwapa jamaa zenu wanacho hitajia, ili kuzidi kutia nguvu makhusiano ya mapenzi kati ya ukoo. Na Mwenyezi Mungu anakataza kutenda kila la makosa, na khasa madhambi yaliyo pita mpaka kwa ubaya, na kila kisicho pendeza katika sharia na akili nzuri. Hali kadhaalika anakataza kumfanyia uadui mtu. Na Mwenyezi Mungu Aliye takasika anakukumbusheni haya, na anakuelekezeni kwenye mambo mema, mpate kukumbuka fadhila zake kwa maelekezo yake mema,basi ndio mfanye anavyo kwambieni.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (90) Sura: An-Nahl
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi