Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Versetto: (81) Sura: Al ‘Imrân
وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ لَمَآ ءَاتَيۡتُكُم مِّن كِتَٰبٖ وَحِكۡمَةٖ ثُمَّ جَآءَكُمۡ رَسُولٞ مُّصَدِّقٞ لِّمَا مَعَكُمۡ لَتُؤۡمِنُنَّ بِهِۦ وَلَتَنصُرُنَّهُۥۚ قَالَ ءَأَقۡرَرۡتُمۡ وَأَخَذۡتُمۡ عَلَىٰ ذَٰلِكُمۡ إِصۡرِيۖ قَالُوٓاْ أَقۡرَرۡنَاۚ قَالَ فَٱشۡهَدُواْ وَأَنَا۠ مَعَكُم مِّنَ ٱلشَّٰهِدِينَ
Na pale Mwenyezi Mungu alipo chukua ahadi kwa Manabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikima, kisha akakujieni Mtume mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juu yenu mumuamini na mumsaidie. Akasema: Je, mmekiri na mmekubali kushika agizo langu juu ya hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema: Basi shuhudieni, na Mimi ni pamoja nanyi katika kushuhudia.
Ewe Nabii! Watajie kuwa Mwenyezi Mungu aliahidiana na akaagana na kila Nabii aliye teremshiwa Kitabu na akapewa ilimu ya manufaa, ya kwamba akija Mtume ambaye wito wake unakubaliana na wito wao basi ni waajibu wao wamuamini na wamsaidie. Na Manabii wote walikiri kuitimiza ahadi hiyo, na wakakiri na wakashuhudia kwa nafsi zao, na Mwenyezi Mungu akawashuhudia hayo. Tena wao wakayafikisha hayo kwa kaumu zao. Ahadi hiyo imewapasia wao imani na wamnusuru wakimwahi. Kama hawakumwahi basi ni waajibu wa kaumu zao wamuamini na wamnusuru kwa kutimiza na kufuata yaliyo walazimu Manabii wao.(Tazama katika Biblia: Kumbukumbu 18.17-19, Injili ya Yohana 16.7-14)
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Versetto: (81) Sura: Al ‘Imrân
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi