Check out the new design

Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Sura: Adh-Dhâriyât   Versetto:

Adh-Dhariyat

وَٱلذَّٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا
Naapa kwa pepo zinazo tawanya!
Ninaapa kwa pepo zinazo timua mawingu, zikayasukuma kwa nguvu, huku zikibeba mizigo mizito ya maji, zikawa zinakwenda kwa wepesi kwa amri ya Mwenyezi Mungu, zikawa zinagawanya riziki kwa ampendaye Mwenyezi Mungu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا
Na zinazo beba mizigo!
Huku zikibeba mizigo mizito ya maji.
Esegesi in lingua araba:
فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
Zikawa zinakwenda kwa wepesi kwa amri ya Mwenyezi Mungu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا
Na zinazo gawanya kwa amri!
Zikawa zinagawanya riziki kwa ampendaye Mwenyezi Mungu.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli!
Hakika hayo mnayo ahidiwa, nayo ya kufufuliwa na mengineyo, ni hakika ya kweli itakayo tokea.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
Na kwamba kwa yakini malipo kwa vitendo vyenu yatakuwa tu hapana hivi wala hivi.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Adh-Dhâriyât
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

La sua traduzione di Ali Muhsin Albirwany.

Chiudi