Check out the new design

وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - عبد الله محمد و ناصر خميس * - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان


وه‌رگێڕانی ماناكان سوره‌تی: یوسف   ئایه‌تی:
فَلَمَّآ أَن جَآءَ ٱلۡبَشِيرُ أَلۡقَىٰهُ عَلَىٰ وَجۡهِهِۦ فَٱرۡتَدَّ بَصِيرٗاۖ قَالَ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ إِنِّيٓ أَعۡلَمُ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Alipokuja mwenye kumpa bishara Ya’qūb kwamba Yūsuf yuko hai, akaitupa kanzu ya Yūsuf usoni mwake akarudi Ya’qūb kuwa yuaona, akajawa na furaha na akawaambia waliokuwa hapo kwake, «Je, sikuwapa habari kwamba mimi nayajua kutoka kwa Mwenyezi Mungu msiyoyajua ya fadhila Zake, rehema Zake na ukarimu Wake.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
قَالُواْ يَٰٓأَبَانَا ٱسۡتَغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَآ إِنَّا كُنَّا خَٰطِـِٔينَ
Wanawe wakasema, «Ewe baba yetu, tuombee Mola wako Atusamehe na Atusitirie dhambi zetu, hakika sisi tulikuwa wakosa katika yale tuliyomfanyia Yūsuf na ndugu yake.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
قَالَ سَوۡفَ أَسۡتَغۡفِرُ لَكُمۡ رَبِّيٓۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
Ya’qūb akasema , «Nitamuomba Mola wangu Awasamehe dhambi zenu, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe dhambi za waja Wake wanaotubia, ni Mwingi wa rehema kwao.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
فَلَمَّا دَخَلُواْ عَلَىٰ يُوسُفَ ءَاوَىٰٓ إِلَيۡهِ أَبَوَيۡهِ وَقَالَ ٱدۡخُلُواْ مِصۡرَ إِن شَآءَ ٱللَّهُ ءَامِنِينَ
Ya’qūb na watu wa nyumbani kwake wakatoka kuelekea Misri wakimkusudia Yūsuf. Walipofika kwake, Yūsuf aliwakumbatia wazazi wake wawili na akawaambia (wao wote), «Ingieni Misri kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu na hali mkiwa mko kwenye amani na mumeepukana na shida, ukame na kila zito.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَرَفَعَ أَبَوَيۡهِ عَلَى ٱلۡعَرۡشِ وَخَرُّواْ لَهُۥ سُجَّدٗاۖ وَقَالَ يَٰٓأَبَتِ هَٰذَا تَأۡوِيلُ رُءۡيَٰيَ مِن قَبۡلُ قَدۡ جَعَلَهَا رَبِّي حَقّٗاۖ وَقَدۡ أَحۡسَنَ بِيٓ إِذۡ أَخۡرَجَنِي مِنَ ٱلسِّجۡنِ وَجَآءَ بِكُم مِّنَ ٱلۡبَدۡوِ مِنۢ بَعۡدِ أَن نَّزَغَ ٱلشَّيۡطَٰنُ بَيۡنِي وَبَيۡنَ إِخۡوَتِيٓۚ إِنَّ رَبِّي لَطِيفٞ لِّمَا يَشَآءُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَلِيمُ ٱلۡحَكِيمُ
Akawakalisha wazazi wake wawili kwenye kitanda cha ufalme wake kwa njia ya kuwatukuza. Na wazazi wake na ndugu zake kumi na moja wakamsalimia kwa kumuinamia kwa kumwamkia na kumtukuza na sio kumuabudu na kumnyenyekea. Na hilo lilikuwa linaruhusiwa katika Sheria yao, na limeharamishwa katika Sheria yetu, kwa ajili ya kuziba njia inayopelekea kwenye ushirikina. Na Yūsuf akamwambia baba yake, «Kusujudu huku ndio uaguzi wa ndoto yangu niliyokusimulia kabla, katika udogo wangu, Mwenyezi Mungu Ameifanya ni kweli. Na amenifadhili aliponitoa jela na akawaleta nyinyi kutoka jangwani, baada ya Shetani kuharibu uhusiano wa undugu baina yangu mimi na ndugu zangu. Hakika Mola wangu ni Mpole wa kupitisha Analolitaka. Yeye Anayajua sana maslahi ya waja Wake, ni Mwingi wa hekima katika maneno Yake na vitendo Vyake.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
۞ رَبِّ قَدۡ ءَاتَيۡتَنِي مِنَ ٱلۡمُلۡكِ وَعَلَّمۡتَنِي مِن تَأۡوِيلِ ٱلۡأَحَادِيثِۚ فَاطِرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ أَنتَ وَلِيِّۦ فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِۖ تَوَفَّنِي مُسۡلِمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّٰلِحِينَ
Kisha Yūsuf alimuomba Mola wake akisema, «Mola wangu! Umenipa ufalume wa Misri, na umnifundisha uaguzi wa ndoto na elimu nyinginezo. Ewe Muumba, na Mtengenezaji, mbingu na ardhi! Wewe Ndiye Msimamizi wa mambo yangu ulimwenguni na Akhera. Nifishe unichukue kwako nikiwa Muislamu na unikutanishe na waja wako wema miongoni mwa Manabii watenda mema na wasafiwa walioteuliwa.»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
ذَٰلِكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهِ إِلَيۡكَۖ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ أَجۡمَعُوٓاْ أَمۡرَهُمۡ وَهُمۡ يَمۡكُرُونَ
Hayo yaliyotajwa ya habari za Yūsuf ni miongoni mwa habari za ghaibu, tunakuelezea , ewe Mtume, kwa njia ya wahyi. Na hukuwako pamoja na ndugu zake Yūsuf walipompangia kumtia kisimani na wakamfanyia hila yeye na baba yake. Hii inaonesha dalili ya ukweli wako na kwamba Mwenyezi Mungu Anakuletea wahyi.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَمَآ أَكۡثَرُ ٱلنَّاسِ وَلَوۡ حَرَصۡتَ بِمُؤۡمِنِينَ
Hawakuwa wengi wa washirikina miongoni mwa watu wako, ewe Mtume, ni wenye kukusadiki wala kukufuata, ingawa una pupa juu ya Imani yao. Basi usisikitike kwa hilo.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
 
وه‌رگێڕانی ماناكان سوره‌تی: یوسف
پێڕستی سوره‌ته‌كان ژمارەی پەڕە
 
وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - عبد الله محمد و ناصر خميس - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

وەرگێڕان: د. عبد الله محمد أبو بكر و شيخ ناصر خميس.

داخستن