Check out the new design

وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - عبد الله محمد و ناصر خميس * - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان


وه‌رگێڕانی ماناكان سوره‌تی: النمل   ئایه‌تی:
۞ فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوۡمِهِۦٓ إِلَّآ أَن قَالُوٓاْ أَخۡرِجُوٓاْ ءَالَ لُوطٖ مِّن قَرۡيَتِكُمۡۖ إِنَّهُمۡ أُنَاسٞ يَتَطَهَّرُونَ
Watu wa Lūṭ hawakuwa na jawabu la kumpa isipokuwa ni kuambiana wao kwa wao, «Watoeni wafuasi wa Lūṭ kwenye mji wenu, kwani wao ni watu wanaojiepusha na kuwajilia wanaume.» Waliwaambia hilo kwa njia ya kuwafanyia shere.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
فَأَنجَيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَٰهَا مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Tukamuokoa Lūṭ na watu wake waliomfuata na adhabu ambayo itawashukia watu wa Lūṭ waliomkanusha, isipokuwa mkewe tuliomkadria kuwa ni mwenye kusalia kwenye adhabu mpaka aangamie pamoja na wenye kuangamia, kwa kuwa yeye alikuwa ni msaidizi wa watu wake kwa matendo yao mabaya na alikua akiridhika nayo.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Na tukawateremshia kutoka mbinguni mvua ya mawe ya udongo yenye kuangamiza. Ilikuwa mbaya mno mvua ya hao walioonywa ambao hoja iliwasimamia.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
قُلِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ وَسَلَٰمٌ عَلَىٰ عِبَادِهِ ٱلَّذِينَ ٱصۡطَفَىٰٓۗ ءَآللَّهُ خَيۡرٌ أَمَّا يُشۡرِكُونَ
Sema, ewe Mtume, «Sifa njema na shukrani ni za Mewenyezi Mungu, na amani kutoka Kwake na usalama ziwashukie waja Wake Aliowateua kwa kuwapa utume.» Kisha waulize washirikina wa watu wako, «Je, Mwenyezi Mungu Anayemiliki kunufaisha na kudhuru ni bora au ni yule wanayemshirikisha badala Yake kati ya wale wasiojimilikia wenyewe wala kuwamilikia wengine nafuu yoyote wala madhara yoyote?»
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَمَّنۡ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَأَنزَلَ لَكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَنۢبَتۡنَا بِهِۦ حَدَآئِقَ ذَاتَ بَهۡجَةٖ مَّا كَانَ لَكُمۡ أَن تُنۢبِتُواْ شَجَرَهَآۗ أَءِلَٰهٞ مَّعَ ٱللَّهِۚ بَلۡ هُمۡ قَوۡمٞ يَعۡدِلُونَ
Na waulize wao , «Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi na Akawateremshia maji kutoka mbinguni, Akaotesha kwa hayo maji mabustani yenye mandhari mazuri?» Hamkuwa nyinyi ni wenye kuipanda miti yake lau si Mwenyezi Mungu kuwateremshia maji kutoka mbinguni. Kumuabudu Mwenyezi Mungu ndio ukweli na kumuabudu asiyekuwa Yeye ndio urongo. Je, kuna muabidiwa pamoja na Mwenyezi Mungu alifanya vitendo hivi mpaka aabudiwe pamoja na Yeye na ashirikishwe na Yeye? Bali washirikina hawa ni watu wanapotoka na njia ya haki na Imani ndio wakamfanya Mwenyezi Mungu ni sawa na asiyekuwa Yeye katika kuabudiwa na kutukuzwa.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَمَّن جَعَلَ ٱلۡأَرۡضَ قَرَارٗا وَجَعَلَ خِلَٰلَهَآ أَنۡهَٰرٗا وَجَعَلَ لَهَا رَوَٰسِيَ وَجَعَلَ بَيۡنَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ حَاجِزًاۗ أَءِلَٰهٞ مَّعَ ٱللَّهِۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Je, kuviabudu vile mnavyovishirikisha na Mola wenu ni bora au Yule Aliyewafanyia ardhi kuwa ni mahali pa kutulia, Akaitoa mito kati yake, Akaiwekea majabali yaliyojikita na Akaweka kizuizi baina ya bahari mbili, ya tamu na chumvi, ili mojawapo isiiharibu nyingine? Je kuna muabudiwa yoyote pamoja na Mwenyezi Mungu alifanya hilo hata mumshirikishe na Yeye katika kuabudu kwenu? Bali wengi wa hawa washirikina hawajui kadiri ya ukubwa wa Mwenyezi Mungu, hivyo basi wanamshirikisha Yeye kwa kuiga na kwa udhalimu.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَمَّن يُجِيبُ ٱلۡمُضۡطَرَّ إِذَا دَعَاهُ وَيَكۡشِفُ ٱلسُّوٓءَ وَيَجۡعَلُكُمۡ خُلَفَآءَ ٱلۡأَرۡضِۗ أَءِلَٰهٞ مَّعَ ٱللَّهِۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Je, kuviabudu vile mnavyovishirikisha na Mwenyezi Mungu ni bora au Yule Anayemjibu mwenye shida anapomuomba, Anayemuondolea maovu yaliyomshukia na Anayewafanya nyinyi ni wenye kushikilia nafasi za waliowatangulia nyinyi katika ardhi? Je, kuna muabudiwa yoyote pamoja na Yeye Anayewaneemesha neema hizi? Ni uchache sana kwenu nyinyi kukumbuka na kuzingatia, na kwa hivyo, mlimshirikisha Mwenyezi Mungu na mwingine katika kumuabudu.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
أَمَّن يَهۡدِيكُمۡ فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِ وَمَن يُرۡسِلُ ٱلرِّيَٰحَ بُشۡرَۢا بَيۡنَ يَدَيۡ رَحۡمَتِهِۦٓۗ أَءِلَٰهٞ مَّعَ ٱللَّهِۚ تَعَٰلَى ٱللَّهُ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Je, kuviabudu vile mnavyomshirikisha navyo Mwenyezi Mungu ni bora au Yule Anayewaongoza katika giza la bara na bahari mnapopotea na njia ikawa na giza kwenu, Ambaye Anapeleka upepo wenye kutoa bishara njema ya kile ambacho Mwenyezi Mungu Anawarehemu waja Wake kwacho, nacho ni mvua yenye kuhuisha ardhi iliyokufa? Je, kuna muabudiwa yoyote pamoja na Mwenyezi Mungu anayewafanyia chochote katika hayo mkamuomba badala yake? Ameepukana Mwenyezi Mungu na kutakasika na hivyo ambavyo wao wanamshirikisha navyo asiyekuwa Yeye.
تەفسیرە عەرەبیەکان:
 
وه‌رگێڕانی ماناكان سوره‌تی: النمل
پێڕستی سوره‌ته‌كان ژمارەی پەڕە
 
وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - عبد الله محمد و ناصر خميس - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

وەرگێڕان: د. عبد الله محمد أبو بكر و شيخ ناصر خميس.

داخستن