وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - علی محسن البرواني * - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

وه‌رگێڕانی ماناكان ئایه‌تی: (50) سوره‌تی: سورەتی یوسف
وَقَالَ ٱلۡمَلِكُ ٱئۡتُونِي بِهِۦۖ فَلَمَّا جَآءَهُ ٱلرَّسُولُ قَالَ ٱرۡجِعۡ إِلَىٰ رَبِّكَ فَسۡـَٔلۡهُ مَا بَالُ ٱلنِّسۡوَةِ ٱلَّٰتِي قَطَّعۡنَ أَيۡدِيَهُنَّۚ إِنَّ رَبِّي بِكَيۡدِهِنَّ عَلِيمٞ
Na mfalme akasema: Mleteni kwangu! Basi mjumbe alipo mjia Yusuf alisema: Rejea kwa bwana wako ukamuulize khabari ya wale wanawake walio jikata mikono yao. Hakika Mola wangu Mlezi anazijua vyema hila zao.
Mfalme akamwona Yusuf atakuwa na faida naye kwa ule uwezo wake kuifasiri ndoto yake, na akaazimia amwite. Akawaamrisha wasaidizi wake wamlete. Alipo mfikia mjumbe akamwabia kuwa mfalme anamtaka, khabari hiyo haikumpapatisha, juu ya kuwa ina bishara ya kufunguliwa kwake. Wala kule kutamani kutoka kwa mfungwa kwenye dhiki za jela na taabu zake hakukuitikisa subira yake. Akakhiari angoje mpaka idhihirike kuwa hana makosa kuliko kufanya haraka kutoka na huku yale aliyo tuhumiwa bado yamemganda. Akamwambia mjumbe: Rejea kwa bwana wako umtake ayaangalie tena yale mashtaka niliyo shitakiwa, awaulize wale wanawake walio kusanywa na mke wa Mheshimiwa kwa kunifanyia hila mimi, wakababaika na wakajikata mikono yao: Je! Walipo toka kwenye yale majaribio walikuwa wanaamini kuwa mimi sina makosa na safi, au waliniona ni mchafu na mzinifu? Mimi nataka haya ipate kuonekana hakika katika macho ya watu. Ama Mola wangu Mlezi anavijua vyema vitimbi vyao!
تەفسیرە عەرەبیەکان:
 
وه‌رگێڕانی ماناكان ئایه‌تی: (50) سوره‌تی: سورەتی یوسف
پێڕستی سوره‌ته‌كان ژمارەی پەڕە
 
وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - علی محسن البرواني - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

وەرگێڕاوی ماناکانی قورئانی پیرۆز بۆ زمانی سواحیلی، وەرگێڕان: علی محسن البرواني.

داخستن