وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - علی محسن البرواني * - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

وه‌رگێڕانی ماناكان ئایه‌تی: (25) سوره‌تی: سورەتی الأنعام
وَمِنۡهُم مَّن يَسۡتَمِعُ إِلَيۡكَۖ وَجَعَلۡنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ أَكِنَّةً أَن يَفۡقَهُوهُ وَفِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَقۡرٗاۚ وَإِن يَرَوۡاْ كُلَّ ءَايَةٖ لَّا يُؤۡمِنُواْ بِهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءُوكَ يُجَٰدِلُونَكَ يَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na wapo miongoni mwao wanao kusikiliza; na tumezitia pazia nyoyo zao wasije kuyafahamu. Na upo uziwi masikioni mwao, na wakiona kila Ishara hawaiamini. Hata wakikujia kwa kujadiliana nawe, wanasema walio kufuru: Hizi si chochote ila hadithi za watu wa kale.
Na miongoni mwao wapo wanao kusikiliza unapo soma Qur'ani, si kwa sababu waifahamu na ipate kuwaongoa, lakini ni kwa ajili wapate njia ya kuitoa kombo na kuikejeli. Na Sisi kwa sababu hiyo tumewazuilia wasiweze kunafiika kwa akili zao na masikio yao. Imekuwa kama kwamba akili zao zimefunikwa haziwezi kuelewa baraabara; na kama kwamba masikio yao yana uziwi unao wazuia wasizisikie Aya za Qur'ani. Na hawa hata wakiona kila dalili hawaamini. Hata wakikujia wakujadili kwa upotovu wanasema walio kufuru, huku wakisukumiza na ukafiri wao: Haya si chochote ila hadithi za uwongo zilizo tungwa na watu wa zamani wa kabla yako!
تەفسیرە عەرەبیەکان:
 
وه‌رگێڕانی ماناكان ئایه‌تی: (25) سوره‌تی: سورەتی الأنعام
پێڕستی سوره‌ته‌كان ژمارەی پەڕە
 
وه‌رگێڕانی ماناكانی قورئانی پیرۆز - وەرگێڕاوی سواحیلی - علی محسن البرواني - پێڕستی وه‌رگێڕاوه‌كان

وەرگێڕاوی ماناکانی قورئانی پیرۆز بۆ زمانی سواحیلی، وەرگێڕان: علی محسن البرواني.

داخستن