Check out the new design

Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Abdullah Muchamed ir Nasir Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Sūra: Ibrahim   Aja (Korano eilutė):

Ibrahim

الٓرۚ كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ إِلَيۡكَ لِتُخۡرِجَ ٱلنَّاسَ مِنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِ بِإِذۡنِ رَبِّهِمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Alif, Lām, Rā. Hii Qur’ani ni kitabu tulichokuletea wahyi ili uwatoe binadamu kutoka kwenye upotevu na upotovu kuwapeleka kwenye uongofu na mwangaza, kwa idhini ya Mola wao na taufiki Yake kwao, kwenye Uislamu ambao ndio njia ya Mwenyezi Mungu Mwenye kushinda Anayehimidiwa kwa kila hali.
Tafsyrai arabų kalba:
ٱللَّهِ ٱلَّذِي لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَوَيۡلٞ لِّلۡكَٰفِرِينَ مِنۡ عَذَابٖ شَدِيدٍ
Mwenyezi Mungu Ambaye ni Vyake vilivyoko mbinguni na vya ardhini, kwa kuviumba, kuvimiliki na kuviendesha. Yeye Ndiye Ambaye ni lazima ibada Afanyiwe Yeye Peke Yake. Na wale waliogeuka na wasimuamini Mwenyezi Mungu na wasiwafuate Mitume Wake watapata maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama.
Tafsyrai arabų kalba:
ٱلَّذِينَ يَسۡتَحِبُّونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا عَلَى ٱلۡأٓخِرَةِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَيَبۡغُونَهَا عِوَجًاۚ أُوْلَٰٓئِكَ فِي ضَلَٰلِۭ بَعِيدٖ
Na hawa wenye kugeuka wasimuamini Mwenyezi Mungu na wasimfuate Mtume Wake ndio wanaochagua maisha ya dunia yenye kutoeka na wanaacha Akhera yenye kusalia, wanawakataza watu kufuata dini ya Mwenyezi Mungu na wanaitaka iwe ni njia iliyopotoka ili iafikiane na mapendeleo yao. Hao waliosifiwa kwa sifa hizi wamo ndani ya upotevu wa kutoiona haki, wako mbali na njia zote za uongofu.
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا بِلِسَانِ قَوۡمِهِۦ لِيُبَيِّنَ لَهُمۡۖ فَيُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Na hatukutuma Mitume kabla yako, ewe Nabii, isipokuwa kwa lugha ya watu wake, ili awafafanulie sheria ya Mwenyezi Mungu, ili Mwenyezi Mungu Apate kumpoteza Anayemtaka awe kando na uongofu na Amwongoze Anayemtaka kwenye ukweli. Na yeye Ndiye Mshindi katika ufalme Wake, ni Mwenye hekima Anayeyaweka mambo mahali pake kulingana na hekima.
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَآ أَنۡ أَخۡرِجۡ قَوۡمَكَ مِنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِ وَذَكِّرۡهُم بِأَيَّىٰمِ ٱللَّهِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّكُلِّ صَبَّارٖ شَكُورٖ
Na kwa hakika tulimtuma Mūsā kwa Wana wa Isrāīl na tukamsaidia kwa miujiza yenye kuonyesha ukweli wake na tukammpa amri awalinganie wao kwenye Imani, ili awatoe wao kutoka kwenye upotevu awatie kwenye uongofu na awakumbushe neema za Mwenyezi Mungu na mateso Yake katika wakati wake. Katika kukumbusha huku mambo hayo kuna dalili nyingi kwa kila mvumilivu sana juu ya utiifu wa Mwenyezi Mungu, kuyaepuka yaliyoharamishwa na Yeye na kuyakubali maandiko Yake, mwenye kushukuru sana, mwenye kusimama kutekeleza haki za Mwenyezi Mungu na anayemshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema Zake. Aina mbili hizi za watu zimetajwa mahsusi, kwa kuwa wao ndio wanaozingatia hizo dalili na hawaghafiliki nazo.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Ibrahim
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Abdullah Muchamed ir Nasir Khamis - Vertimų turinys

Išvertė Dr. Abdullah Muchamed Abubakar ir šeichas Nasir Khamis.

Uždaryti