Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (222) Sūra: Sūra Al-Bakara
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡمَحِيضِۖ قُلۡ هُوَ أَذٗى فَٱعۡتَزِلُواْ ٱلنِّسَآءَ فِي ٱلۡمَحِيضِ وَلَا تَقۡرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطۡهُرۡنَۖ فَإِذَا تَطَهَّرۡنَ فَأۡتُوهُنَّ مِنۡ حَيۡثُ أَمَرَكُمُ ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلتَّوَّٰبِينَ وَيُحِبُّ ٱلۡمُتَطَهِّرِينَ
Na wanakuuliza kuhusu hedhi, nayo ni damu inayotiririka kimaumbile kutoka kwenye uzao wa wanawake katika nyakati maalumu.Waambie, ewe Mtume, «Hiyo hedhi ni udhia wenye manyezi unaomdhuru mwenye kuusongelea. Hivyo basi, jiepusheni kuwaingilia wanawake kwenye kipindi cha hedhi mpaka damu ikome. Damu ikomapo, na wakaoga, waingilieni kupitia pale pahali Alipowahalalishia Mwenyezi Mungu, napo ni tupu ya mbele siyo ya nyuma. Hakika Mwenyezi Mungu Anawapenda waja Wake wenye kutubia na kuomba msamaha kwa wingi na Anawapenda waja Wake wenye kujisafisha ambao hujitenga na maovu na uchafu.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (222) Sūra: Sūra Al-Bakara
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti