Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (258) Sūra: Sūra Al-Bakara
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِي حَآجَّ إِبۡرَٰهِـۧمَ فِي رَبِّهِۦٓ أَنۡ ءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ إِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّيَ ٱلَّذِي يُحۡيِۦ وَيُمِيتُ قَالَ أَنَا۠ أُحۡيِۦ وَأُمِيتُۖ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَأۡتِي بِٱلشَّمۡسِ مِنَ ٱلۡمَشۡرِقِ فَأۡتِ بِهَا مِنَ ٱلۡمَغۡرِبِ فَبُهِتَ ٱلَّذِي كَفَرَۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Je umewahi kuona, ewe Mtume, hali ya kustaajabisha zaidi kuliko ile ya yule aliyemjadili Ibrāhīm, amani imshukie, juu ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na juu ya uola Wake, kwa kuwa Mwenyezi Mungu Alimpa ufalme, alipofanya ujeuri na kumuuliza Ibrāhīm, «Ni nani Mola wako?» Alisema, amani imshukie, «Mola wangu ni Ambaye Anavipa viumbe uhai vikahuika na Anaviondolea uhai vikafa. Yeye Ndiye Aliyepwekeka kwa kuhuisha na kufisha.» Akasema, «Mimi nahuisha na kufisha.» Yaani: namuua nimtakaye kumuua, na namuachilia nimtakaye kumuachilia. Ibrāhīm akasema kumwambia, «Mwenyezi Mungu ninayemuabudu Analitoa jua upande wa mashariki. Je unaweza wewe kugeuza mwenendo huu wa kimungu, ulifanye litokeze upande wa magharibi?» Akapigwa na mshangao huyu kafiri na ikakatika hoja yake. Hali yake ni ile ya madhalimu, Mwenyezi Mungu Hawaongozi kwenye haki na usawa.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (258) Sūra: Sūra Al-Bakara
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti