Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (101) Sūra: Sūra Al-Ma’idah’
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَسۡـَٔلُواْ عَنۡ أَشۡيَآءَ إِن تُبۡدَ لَكُمۡ تَسُؤۡكُمۡ وَإِن تَسۡـَٔلُواْ عَنۡهَا حِينَ يُنَزَّلُ ٱلۡقُرۡءَانُ تُبۡدَ لَكُمۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهَاۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Enye ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu, Mtume wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, msiulize mambo ya Dini ambayo hamkuamrishwa chochote kuhusu hayo, kama kuuliza kuhusu mambo ambayo hayajatukia au yale ambayo yatapelekea mikazo ya Sheria ambayo lau mlikalifishwa nayo yangalikuwa ni magumu kwenu, na lau mliyauliza wakati wa uhai wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,, wakati Qur’ani inateremka, mungalielezewa, na pengine mkakalifishwa nayo na mkalemewa nayo. Hayo Mwenyezi Mungu Ameyaacha ili kuwapumzisha waja Wake nayo. Na Mwenyezi Mungu ni Msamehefu sana kwa waja wake wanapotubia, ni Mpole sana kwao, Hawaadhibu wakirudi Kwake.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Aja (Korano eilutė): (101) Sūra: Sūra Al-Ma’idah’
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti